Taasisi ya isiyo ya Kiserikali inayojishughulisha na maswala ya Mazingira pamoja na Utu (HDIECA) , iliandaa maonesho maalum ambayo yaliwakutanisha wajasiliamali mbalimbali ambao wanafanya shughuli zao kwa kutumia mikono yao kwa lengo la kurudisha shukurani zao kwa jamii kutokana na wananchi kupokea na kushirikiana nao vyema katika kazi zao mbalimbali wanazozifanya kila siku.
Maonesho hayo yalifanyika katika viwanja vya Azura Kawe Jijini Dar es Salaam na hakukuwa na kiingilio chochote kwa wananchi na wajasiliamali hawakulipia kitu ilikuwa ni Bure kabisa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wajasiliamali wengi waliishukuru taasisi hivyo kwa kuwapa fursa hiyo hata ya kuonesha kazi zao na kufahamiana na watumbalimbali na pia kuongeza wigo wa kibiashara kwa kupata wateja wapya.
Katika maonesho hayo kulikuwa na wajasiliamali wanaotengeneza vitu mbalimbali kwa mikono yao ambapo pamoja na yote waliomba ikiwezekana watengewe sehemu ambayo watakuwa wanapeleka bidhaa zao na kuziuza hata mara moja kwa mwezi.
Wananchi wakiendelea kutazama Bidhaa mbalimbali zilizotengenezwa na watanzania .
Wajasiliamali mbalimbali pamoja na waandaaji wa maonesho hayo wakiwa katika picha ya pamoja
Moja ya Banda la mjasiliamali anayetengeneza Batiki
Moja ya Banda la mjasiliamali anayetumia chupa chakavu zilizotupwa anaokota na kuziongezea thamani kwa kuviwekea marembo kwa kutumia nyuzi vitambaa na nakshi nakshi zengine
Moja ya Banda la mjasiliamali anayetengeneza bidhaa zao kwa kutumia mishumaa na maua ya asili
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...