Asteria Muhozya na Rhoda James, GEITA.

 Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Madini imeanza kufanya mazungumzo na nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ili iweze kujenga Kiwanda cha Kuchenjua madini ya Colbat nchini.
 Hayo yalibainishwa Oktoba 19, mkoani Geita  na Waziri wa Madini wa Tanzania Angellah Kairuki wakati wa kuhitimisha ziara ya siku Nne ya  Waziri wa Madini wa Kongo (DRC), Martin Kabwelulu aliyoifanya nchini kwa mwaliko wa Waziri Kairuki.

Kairuki alisema kuwa, nchi ya Kongo ndiyo mzalishaji mkubwa wa madini ya Colbat duniani ambapo asilimia 70 ya madini hayo duniani yanazalishwa nchini humo.Aliongeza kuwa, kwa sasa nchi hiyo inayo changamoto ya kusafirisha madini hayo yakiwa ghafi ikiwemo ukosefu wa umeme wa kutosheleza kwa ajili ya ujenzi wa viwanda hivyo.

“Tumekubaliana kuendelea na mazungumzo  na Kongo ili shughuli za uchenjuaji na uyeyushaji wa madini hayo ufanyike nchini  kwa kuwa tumeshaanza kuwekeza kwenye Vinu/viwanda  vya Kuchenjua na kuyeyusha madini mbalimbali. Hivyo, tunataka wayasafirishe makinikia ya Colbat hapa na tuyachenjue hapa,” alisisitiza Kairuki.

Akizungumzia matumizi ya madini hayo, Kairuki alisema kuwa, madini ya Colbat yanatumika kutengeneza betri na vihifadhi nishati (capacitor) ambazo zinahitajika sana hususan, kwenye magari yanayotumia umeme.bali na makubaliano ya ujenzi wa kiwanda hicho, pia Waziri Kairuki alisema kuwa nchi hizo zimekubaliana masuala kadhaa ikiwemo kuendelea kubadilishana uzoefu wa usimamizi wa sekta ya Madini ili kuweza kunufaisha wananchi hasa wale wanaozunguka maeneo ya migodi.
 
 Waziri wa Madini Angellah Kairuki na mgeni wake Waziri wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) Martin Kabwelulu (wa pili kushoto) wakimsikiliza Mtaalam Mwelezi  Martin Sezinga Akiwaonesha mashine mbalimbali zinazotumiwa katika hatua mbalimbali za uzalishaji na uchenjuaji wa madini ya dhahabu katika mgodi wa mfano wa Lwamgasa.
PICHA 2- BUSOLWA
Waziri wa Madini Angellah Kairuki (kushoto) na Waziri wa  Madini wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Martin Kabwelulu wakiteta jambo baada ya kutembelea mgodi wa Busolwa Mining Ltd unaomilikiwa na Mtanzania, mkoani Geita
PICHA 3 KONGO TANZANIA
Meneja wa Mgodi wa Busolwa Mining Ltd, Flex Adoph akimweleza jambo Waziri wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Martin Kabwelulu (katikati) wakati alipotembelea katika mgodi huo kujifunza namna mmiliki wa mgodi huo alivyotoka katika uchimbaji mdogo hadi kuwa mchimbaji wa Kati lakini pia kujifunza namna mgodi huo unavyofanya shughuli zake za uchenjuaji na uzalishaji wa madini ya dhahabu. Anayeshuhudia ni Waziri wa Madini Angellah Kairuki.
PICHA 5 B
Waziri wa Madini wa  Angellah Kairuki na Mgeni wake Waziri wa Madini wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Martin Kabwelulu (Wa tatu kushoto) wakiangalia madini ya Dhahabu yanayozalishwa na kuchenjuliwa katika Mgodi wa Nsangano Gold Mine mkoani Geita walipoutembelea mgodi huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...