Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii 
MAMLAKA ya chakula na dawa nchini (TFDA) kwa kushirikiana na shirika la Viwango nchini (TBS) , Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) chama cha mawakala wa forodha nchini (TAFFA) wamekutana na kujadili namna ya kuimarisha na suala zima uingizaji wa bidhaa nchini. 

Akizungumza katika mkutano huo kaimu mkurugenzi mkuu wa TFDA Agnes Kijo ameeleza lengo la mkutano huo ni kukumbushana ili kuweza kusaidia kuboresha huduma kwenye taasisi hizo katika utoaji wa mizigo kwa kufuata sheria kwani bila kufanya hivyo hawatafikia malengo ya taifa. 

Amesema kuwa waingizaji wa mizigo na mawakala wa forodha lazima wawe pamoja katika kulinda afya za wananchi. 

Ameeleza kuwa wamekaa na wadau wengi wakimemo wenye viwanda na awamu hii wameamua kukaa na mawakala hao wa uingizaji mizigo nchini ili kubaini changamoto zinazowakabili na kuweza kuzitatua na kuongeza ufanisi katika utendaji kazi wao. 

Agnes ameeleza kuwa wote wapo kwa ajili ya kuijenga nchi hivyo ni lazima kuhakikisha kila mamlaka inasimamia ipasavyo majukumu yao ili kuhakikisha kuwa suala la uingizaji wa mizigo kwa kuzingatia umuhimu wa wadau hao na amehaidi kuwa taratibu zitaenda kufanyika kielektronoki ili kurahisisha mchakato mzima. 

MKemia Mkuu wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali ,Mkuu wa Serikali Dkt. Fidelince Mafumiko amesema kuwa mkutano huo ni muhimu kwa wadau hao hasa katika uingizaji wa kemikali kwa ajili ya viwanda na ameeleza kuwa wadau hao ndio huwezesha uingizwaji wa bidhaa hizo hivyo ni fursa kwao katika kutoa taratibu na mrejesho wa changamoto katika kutekeleza ufanisi, na changamoto zitakazotolewa na wadau watazifanyia kazi na amesema kuwa huo ni mwanzo mzuri katika utoaji wa huduma. 

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa shirika la viwango (TBS) Lazaro Msasalaga amesema kuwa lengo la mkutano huo ni kuongeza ufanisi katika mchakato wa utoaji wa mizigo bandarini pamoja na changamoto zinazogusa taasisi zao na kuendeleza uchumi wa nchi. 
Kaimu Mkuruergnzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Agnes Kijo akizungumza na wadau wa wakala forodha katika mkutano wa kujadili masuala mbalimbali ya utaoaji wa huduma katika bandari kwa bidhaa za vyakula uliofanyika jijini Dar es Salaam. 
Mkemia Mkuu wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt. Fidelice Mafumiko akizungumza na vyombo vya habari wakati wa mkutano wa uliowahusisha wakala wa uingizaji wabidhaa ndani ya nchi kupitia kwa mawakala wa forodha juu ya uingizaji wa bidhaa hizo na mamlaka za utoaji wa vibali uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. 
Baadhi ya washiriki katika mkutano wa wadau wa forodha katika mkutano wa ulioitishwa na TFDA kwa ajili ya uboreshaji wa huduma katika uondoshaji wa mizigo katika bandari.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...