Wananchi wa jimbo la Liwale wamepongezwa kwa kujitokeza kwa wingi na mapema kwenda kupiga kura kuwachagua viongozi wanaowataka,
Hayo yameelezwa na Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Balozi Ramadhani Mapuli akiwa anafuatili uchaguzi mdogo katika Jimbo la Liwale.
Balozi Mapuli amesema kwamba, ameridhishwa na utaratibu wa upigaji wa kura ikiwa ni pamoja na vituo kufunguliwa kwa wakati na hakuna malalamiko yoyote yaliyojitokeza katika hatua za awali.
Amewasihi wakazi wa Jimbo hilo kuendelea kujitokeza kwa wingi na kupiga kura katika hali ya amani na utulivu.
Kwa mujibu wa Mkurugezi wa uchaguziJimbo la Liwale Luiza Mlelwa amesema kuwa Jimbo hilo lina wapiga kura 55,777 na Vituo vya kupigia kura 158.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...