Na Judith Mhina – MAELEZO

Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Dkt Detlef Waechter amempongeza Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli kwa kufanikiwa kupambana na rushwa nchin Tanzania na kupata mafanikio makubwa ndani ya kipindi kifupi.

Hayo amesema Balozi Waechter alipofanya mahojiano na Idara ya Habari MAELEZO mapema jana katika hoteli ya Hyatt Regency The Kilimanjaro Dar-es-salaam Kempinski katika barabara ya Sokoine Jijini Dar-es –salaam.

Akielezea jinsi rushwa ilivyoota mizizi sehemu nyingi ikiwemo Ujerumani amesema “Tatizo la rushwa sio la Tanzania peke yake, hata pale Ujerumani lipo japo si kwa kiasi kikubwa, bali kila mara serikali inapaswa kujiangalia na kuhakikisha inapambana na mfumo wa rushwa mahala popote. Ili raia wako wawe na imani na serikali yako”

Kwa dhati kabisa nampongeza Rais Magufuli kwani hali ilikuwa sio nzuri kulingana na ripoti tuliyoisikia wakati wa Mkutano wa 38 wa Bara la Afrika wa Kuthibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya miezi mawili iliyopita. Uwepo wa rushwa Tanzania ilikuwa ni eneo linalotumiwa katika kupitisha madawa hayo ambapo sasa suala hili limepungua kwa kiasi kikubwa kutokanana juhudi za Rais Magufuli.

Akielezea ubaya wa rushwa Balozi Waechter amesema kuwa matatizo ya rushwa yanarejesha nyuma maendeleo kwa kuwa watu hawapati huduma wanazostahili kwa kuwa tu kuna wengine wanatumia rushwa. Halikadhalika uwepo wa rushwa unaondoa uaminifu kutoka Taifa moja kwenda linguine au nchi moja kwenda nyingine.

Ukiangalia maeneo ambayo hayana utulivu na amani, inatokana na kushamiri kwa rushwa na kuwa na serikali ambazo hazisimamii vema huduma kwa wananchi wake. Hili ni tatizo kubwa lililokumba nchi za kiafrika ambazo raia wake kila siku wanatafuta njia ya kuelekea Ulaya.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...