Na. Benedict Liwenga-TRA. 

WAFANYABIASHARA Mkoani Songwe wametakiwa kujitokeza kwa katika Kampeni ya Usajili na Elimu kwa Mlipakodi inayoendeshwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). 

Kauli hiyo imetolewa leo na Afisa Kiongozi wa Kituo cha Huduma cha TRA mjini Tunduma wakati wa Kampeni ya Usajili na Elimu kwa Walipakodi mkoani hapo ambapo amewataka Wafanyabiashara kujitokeza kwa wingi kuweza kupatiwa huduma hiyo pasipo gharama yoyote. 

Bwana Mwita ameeleza kuwa, mwitikio wa wafanyabiashara katika kampeni hiyo ni mkubwa, ambapo wengi wa Wafanyabiashara ambao walikuwa hawana Namba ya Utambulisho ya Mlipakodi (TIN) wameshasajiliwa na kupatiwa TIN hizo. 

“Zoezi hili ni zuri na mwitikio wa watu ni mkubwa, niwaombe Wafanyabiashara waendelee kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kupatiwa TIN na elimu kuhusu masuala ya kodi”, alisema Mwita. 

Kwa upande wake Kiongozi wa msafara kutoka TRA Makao Makuu ambaye pia ni Afisa Mkuu Mwandamizi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi, Bi. Rose Mahendeka amesema kwamba, zoezi la usajili na utoaji elimu kwa mlipakodi litadumu mkoani Songwe kwa muda siku sita, ambapo wafanyabiashara wanahimizwa kuchangamkia fursa hiyo ili waweze kutatua kero mbalimbali zinazowakabili. 

“Kampeni hii katika Mkoa huu wa Songwe litadumu kwa muda wa siku sita na tayari tumeshaanza na maeneo mbalimbali kama vile Vwawa, Mlowo, Tunduma na baadaye tunaendelea na maeneo ya Mkwajuni, Ileje pamoja na Saza lengo ni kuwahamasisha wananchi hususan wafanyabiashara kuitikia wito wa kampeni hii”, alisea Mahendeka. 
 Afisa Mkuu Mwandamizi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bi. Rose Mahendeka (kushoto) akiwaeleimisha baadhi ya Wafanyabiashara wa Tunduma wakati wa Kampeni ya Usajili na Elimu kwa Mlipakodi inayoendelea Mkoani Songwe. 
 Baadhi ya Wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) (kushoto) wakiwasajili na kuwapatia elimu ya kodi Wafanyabiashara wa Tunduma wakati wa Kampeni ya Usajili na Elimu kwa Mlipakodi inayoendelea Mkoani Songwe.(PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-TRA).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...