WAJASILIAMALI,wafugaji wa kuku na wadau wa nyama hapa nchini wameaswa kufatilia masuala ya ufugaji kwa kuwa ufugaji unafursa nyingi hapa nchini.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa  ukuzaji biashara wa mamlaka ya maendeleo ya biashara Tanzania (TanTrade) Boniface Michael wakazi akizungumza na MICHUZIBLOG jijini Dar es salaam leo.

 Amesema kuwa maonyesho hayo  nikwaajili ya kukuza biashara na kutafuta masoko ya bidhaa zinazozalishwa hapa nchini katika masoko ya ndani, kikandana kimataifa.

Michael amesema kuwa maonyesho hayo yanayofanyika jijini Dar es Salaam yapo kwaajili ya kuwaunganisha wazalishaji wa ndani ya nchi na masoko ya kimataifa pamoja na ya kikanda.

Amesema kuwa TanTrade wanakuza biashara za watengenezaji wa bidhaa mbalimbali kwa kuonyesha kupitia maonyesho ya kikanda.
Amema kuwa maonyesho hayo yaliyoanza Oktoba 12 na 13 jijini Dar es Salaam lametoa fursa kwa jamii kujipatia elimu ya ufugaji wa kuku bila gharama yeyote.
Kaimu Mkurugenzi wa  ukuzaji biashara wa mamlaka ya maendeleo ya biashara Tanzania (TanTrade) Boniface Michael  akizungumza na MICHUZI BLOG mara baada ya kutemelea maonyesho ya kuku yaliyofanyika katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wananchi wakijipatia elimu kutoka kwa wafugaji wa kuku na wadau wa nyama hapa nchini katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam leo.

 Wananchi wakipata maelezo jinsi ya ufugaji kuku kwa kisasa zaidi hapa nchini katika maonesho ya kuku yanayofanyika katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
 Banda la vyakula vya kuku katika viwanja vya maonyesho sabasaba jijini Dar es Salaaam.
Picha na Avila Kakingo globu ya Jamii

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...