Na. Vero Ignatus , Liwale-Lindi

Wananchi wa Liwale na viunga vyake wamejitokeza kwa wingi asubuhi ya leo katika vituo vya kupigia kura kwenye uchaguzi mdogo wa Ubunge 2018 mkoa wa Lindi.

Kwa mujibu wa Msimamizi wa uchaguzi jimbo la Liwale Luiza Mlelwa amesema jumla ya wapiga kura waliojiandikisha 55777 na vituo vya kupigia kura 158 wote hawa watapiga kura kumchagua mbunge wao pamoja na diwani kata ya Kibutuka

Balozi Ramadhani Mapuri mjumbe wa Tume ya Taifa ya uchaguzi amesema kuwa ameshuhudia ufunguzi wa vituo, ambapo wapiga kura wamejitokeza kwa wingi na zoezi limeanza kwa wakati hivyo wananchi wasisite kwenda kupiga kura kwani uchaguzi unaendeshwa kwa Amani na Utulivu

Amesema katika vituo vya kupigia kura vya Likongowele Galani pamoja na Kituo cha Ujenzi hali ya uchaguzi ni shwari na wananchi wameendelea kujitokeza kwa wingi kupiga kura.

Wananchi hao wanapiga kura kuwachagua viongozi wanaowapenda kutoka vyama mbalimbali vya siasa, Abduli Kombo Ngakolwa kutoka chama cha wakulima AAFP, Hamis Mohamed Lihindi kutoka ACT Wazalendo, Kachauka Zuberi Mohamed (CCM) Mtesa Mohamed Rashid (CUF) na Mwajuma Noty Mirambo (UMD).
Balozi Ramadhani Mapuri mjumbe wa Tume ya Taifa ya uchaguzi akiwa katika Kitio cha kupigia kura cha Ujenzi. Picha na Vero Ignatus. 
Pichani ni foleni ya kupiga kura katika kituo cha Likongowele Galani leo asubuhi Wilaya ya Liwale Mkoani Lindi. Picha na Vero Ignatus. 
Mmoja ya mwananchi kama anavyooneka tayari ameshapiga kura leo asubuhi. Picha na Vero Ignatus. 
Upigani kura ukiendelea kama inavyoonekana Pichani wananchi wakiwa kwenye foleni. Picha na Vero Ignatus
Wananchi wakiwa katika kituo cha kupigia kura Likongowele ghalani katika Jimbo la Liwale Mkoani Lindi leo asubuhi 13 Octoba 2018, Picha na Vero Ignatus. 
Hapa ni kituo cha kupiga kura cha Ujenzi wananchi wakiwa kwenye foleni tayari kwa kupiga kura leo asubuhi. Picha na Vero Ignatus. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...