WANANCHI wa Kata Magawa wilayani Mkuranga wamelalamikia kuingia kwa wanawake wanaouza miili yao (Madada poa) kwa kutumia mazao.
Wananchi hao wamesema ujio wa wanawake ni katika kipindi cha mauzo ya msimu wa Korosho na Nazi ndio wanaingia na kuanza kufanya biashara ya ngono.
Wamesema wanawake hao wanachukua debe moja ya kurosho kwa wanaume kwa ajili ya kufanya ngono au kutoa Nazi 10 hadi 15.
Akizungumza na Michuzi Blog Mariam Hamis amesema kuwa ujio wanawake hao imekuwa kero katika ndoa zao.
Amesema kuwa serikali ya wilaya isipowatoa watakwenda wenyewe kupambana nao hata kwa mapanga.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkuranga Juma Abeid amesema kuwa suala hilo kwa Mkuu wa Wilaya.
Abeid amesema amesema ujio wadada hao ni changamoto katika kuambukizana na magonjwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...