WANANCHI wa Kata Magawa wilayani Mkuranga wamelalamikia kuingia kwa wanawake wanaouza miili yao (Madada poa) kwa kutumia mazao.

Wananchi hao wamesema ujio wa wanawake ni katika kipindi cha mauzo ya msimu wa Korosho na Nazi ndio wanaingia na kuanza kufanya biashara ya ngono.

Wamesema wanawake hao wanachukua debe moja ya kurosho kwa wanaume kwa ajili ya kufanya ngono au kutoa Nazi 10 hadi 15.

Akizungumza na Michuzi Blog Mariam Hamis amesema kuwa ujio wanawake hao imekuwa kero katika ndoa zao.

Amesema kuwa serikali ya wilaya isipowatoa watakwenda wenyewe kupambana nao hata kwa mapanga.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkuranga Juma Abeid amesema kuwa suala hilo kwa Mkuu wa Wilaya.

Abeid amesema amesema ujio wadada hao ni changamoto katika kuambukizana na magonjwa. 
Amesema kila msimu wa korosho wanawake hao wamekuwa wakiweka kambi.Mwenyekiti wa halmashaul ya Wilaya Mkuranga na Diwani wa kata ya Magawa,Juma Abed akizungumza na michuzi blog juu ya changamoto ya uwepo wa dada poa katika kata yake.
Picha na Emmaniel Massaka wa Global ya jamii)
Wakazii wa kata ya Magawa Wilaya ya mkuranga mkoa Pwani wakizungumza na michuzi blog juu ya ambapo wameiomba serikali iwasaidie kuondoa dadapoa abapo huwa napiga gambi kilaunapofika msimu wa wa korosho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...