*Amuagiza mkuu wa wilaya afanye uchunguzi kubaini zinapokwenda

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Bw. Jabir Shekimweri afanye uchunguzi kuhusu matumizi ya sh. milioni 70 zinazotelewa kila mwezi na Serikali kwa ajili ya kununulia dawa kwenye wilaya hiyo.

"Kilichokuwa kinasemwa na wabunge bungeni nilidhani sicho, nikasema nakuja niyasikie mwenyewe. Kweli wananchi hawaridhiki nimeona. Sasa mkuu wa wilaya shughulikia hili jambo ili kubaini fedha za dawa zinakwenda wapi.”

Alitoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Oktoba 10, 2018) wakati akihutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule msingi Mpwapwa, ambapo alipokea malalamiko ya wananchi juu ya ukosefu wa dawa. Dawa pekee wanazopewa ni za kutuliza maumivu tu.

Waziri Mkuu alisema lengo la Serikali kutoa fedha hizo kila mwezi ni kuhakikisha kwamba wananchi wote wanapata huduma za afya popote walipo badala ya kusafiri umbali mrefu kwenda makao makuu ya wilaya.

"Kila mwezi Serikali inatoa zaidi ya sh milioni 70 kwa ajili ya kununulia dawa kwenye wilaya hii ya Mpwapwa. Pia kuna fedha za mfuko wa afya sh. milioni 60 pamoja na fedha za matokeo mazuri ya afya sh. milioni 300 kwa mwaka, shida ya dawa haitakiwi kuwepo hapa.”
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Mpwampwa, kwenye ukumbi wa chuo cha uwalimu Mpwapwa mkoani Dodoma, Oktoba 10, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mpwampwa Paul Mamba Sweya, kwenye ukumbi wa chuo cha uwalimu Mpwapwa mkoani Dodoma, Oktoba 10, 2018.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwahutubia wananchi wa Wilaya ya Mpwapwa kwenye uwanja wa Chazugwa mkoani Dodoma, Oktoba 10, 2018. 
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega, akizungumza na wananchi wa Mpwapwa katika uwanja wa Chazugwa mkoani Dodoma, Oktoba 10, 2018.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa na mkewe Marry, akikagua shamba la korosho la Magereza wilayani Mpwapwa Dodoma, Oktoba 10, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...