Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) Injinia Patrick Mfugale (kushoto) akimwelezea Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Issack Kamwele (kulia) maendeleo ya mradi wa ujenzi wa barabara sita kutoka Dar es Salaam hadi Maili Moja Kibaha unaojengwa na fedha za Serikali kwa gharama ya takribani zaidi ya shilingi bilioni 140.
Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Julius Ndyamukama (aliye nyoosha kidole) akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Issack Kamwele alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara sita kutokea Dar es Salaam hadi Mail Moja Kibaha.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe pamoja na msafara wake wakitembelea mradi wa barabara sita unaoendelea eneo la Kimara Dar es Salaam hadi Mail Moja Mkoa wa Pwani.
Ujenzi wa barabara sita kutokea Dar es Salaam hadi Mail Moja Kibaha ukiendelea. Eneo hili unajengwa ukuta kuzuia maji ya mto kuingilia barabara hizo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...