Baadhi ya vijana ambao wanashiriki kampeni hiyo ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya watoto mkoani Iringa zoezi ambalo linaenda sambamba na utoaji elimu ujasiriamali kupitia michezo.

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.
ZAIDI ya watoto 1,300 wamejuishwa katika kampeni ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya watoto mkoani 


Iringa zoezi ambalo linaenda sambamba na utoaji elimu ujasiriamali kupitia michezo.

Mratibu wa mradi wa kuwawezesha wasichana kiuchumi uliochini ya shirika la BRAC Anna David amewaambia waandishi wa Habari katika viwanja vya chuo kikuu kishiriki cha elimu Mkwawa (MUCE)  

kuwa lengo la kufanya michezo hiyo kuwaleta pamoja watoto kutoka pande mbalimbali na kuwapa elimu juu ya kupinga ukatili kwa wasichana siku chache kabla ya kufikia maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike yatakayofanyika baadae Octoba 11 mwaka huu katika viwanja vya mwembetogwa mjini Iringa.

Bi David alisema katika maadhimisho hayo Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Salum Hapi anatarajia kuwa mgeni rasmi, maamisho ambayo siku ambayo vilevile ulimwengu unaadhimisha.

Mratibu wa mradi huo alisema waliamua kuijumuisha mkoa wa Iringa baada ya kuona unakabiliwa na visa vya ukatili na hadi sasa wamekwisha kuunda klabu zipatazo 50 ambazo zimekuwa zikitumika kutoa elimu ya kupingana vitendo vya ukatili, ujasiriamali ,kuibua vipaji vya watoto ,kuwafundisha namna ya kuweka fedha na kujiajiri.

Mashindano hayo yameshirikisha watoto wa shule za msingi,sekondari na baadhi ya watoto ambao wameshindwa kuendelea na masomo yao kwa sababu tofauti.

Alisema kuwa kupitia michezo chini ya mwavuli wa shirika lisilo la kiserikali la BRAC wamepeleka zaidi ya watoto 160 chuo cha veta kwa ajaili ya kujifunza ujasiriamali.

Nao baadhi ya washiriki wa michezo hiyo Sarafina Mwinuka alisema kuwa amepata elimu ambayo itamsaidia kuepuka na mambo yasiyofaa ikiwamo usinzi,ndoa na mimba za utotoni.

Naye agetine Joseph na Neema Pius walisema kuwa wanajifunza stadi mbalimbali za maisha ikiwamo kuweka akiba,kujitambua na michezo hiyo imefanyika ikiwa wanaadhimisha siku 16 za kupinga ukatili kwa watoto.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...