Seriklai imeziagiza Mamlaka ya Udhiti Ubora Tanzania (TBS), Mamlaka ya Udhiti wa ubora wa Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) na SIDO kuwapa elimu Wanawake wajasiliamali wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro ili kuongezea thamani katika bidhaa zao kwa kuwapa wabunifu na kuhakikisha bidhaa zao zinakuwa vifungashio vyenye ubora ili ziweze kushindana katika soko na bidhaa nyingine.

Hayo yamesemwa mkoani Morogoro Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati alipotembelea vikundi vya wanawake wajasiliamali wa Wilaya ya Mvomero katika ziara yake Mkoani Morogoro kuangalia utoaji huduma za Afya na Maendeleo ya Jamii.

Pamoja na mambo mengine Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Ndugulile amesema ili wanawake hao waweze kufikia malengo yao na kukuza biashara yao lazima bidhaa ziwe na nembo ya biashara ambayo itatambulisha bidhaa zao na kusaidia kuvutia wateja.

‘’Wekeni nembo katika bidhaa zenu na serikali ya Wilaya iwasaidie ili muweze kuwa na viwanda vidogo vya uzalishaji mali jambo ambalo lipo pia katika Nchi zinazoendelea ambapo viwanda vidogo vimekuwa vikisaidia kuinua hali ya maisha ya wananchi mfano mkiongezea thamani bidhaa zenu na kuzipa nembo ya Movomero itakuwa bora zaidi’’. Alisisitiza Dkt. Ndugulile.


Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongozana na Wananchi wa kijiji cha Wami Luwindo kilichopo Dakawa Wilaya ya Mvomero kukagua mradi wa skimu ya umwagiliaji uanondeshwa na Serikali ya kijiji hicho. 
Wajasiliamali wadogo kutoka vikundi vya mbalimbali vilivyopo wilayani Mvomero wakitoa maelezo kuhusu bidhaa wanazozalisha kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipotembelea Wilaya hiyo jana kujionea kazi za vikundi hivyo wakati wa ziara yake ya siku tatu Mkoani humo. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikabidhi milioni moja kwa Mwenyekiti Skimu ya Umwagiliaji wa kijiji cha Wami Luwindo kilichopo Dakawa Wilaya ya Mvomero Bw. Juma Achumu kama mchango wa Wizara yake kuwezesha na kuamsha hari ya Wananchi kijiletea maendeleo. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW .


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...