Katika mechi ya nne ya hatua ya makundi kwenye ligi ya EUROPA Alhamisi hii timu ya Arsenal itakuwa nyumbani katika dimba la Emirates dhidi ya Sporting CP ya Ureno. Katika mchezo wao wa mzunguko wa kwanza Arsenal waliibuka na ushindi wa bao 1 ambao uliwawezesha kuwa vinara na kuongoza kundi E.
Arsenal wamekuwa katika kiwango bora na wanacheza kandanda safi tangu wampate kocha Unai Emery ambaye amebadilisha aina ya uchezeji wake. Mchezo huo utachezwa Alhamisi tar 8 Novemba, majira ya saa 5:00 Usiku saa za Afrika Mashariki na utarushwa moja kwa moja kupitia chaneli ya ST World Football katika king’amuzi cha StarTimes.
Katika Usiku huo wa EUROPA mechi nyingine zitakazochezwa ni pamoja na ule wa Chelsea ambao watakuwa ugenini dhidi ya BATE Borisov (saa 2:55 Usiku), Fenerbahce vs Anderlecht (saa 12:50 jioni), Lazio vs Olympique Marseille (saa 2:55 Usiku), Celtic vs RB Leipzig (saa 5:00 Usiku) na Real Betis vs AC Milan (saa 5:00 Usiku), yote kupitia chaneli za michezo za StarTimes.
Michuano ya EUROPA inaonyeshwa kupitia king’amuzi cha StarTimes pekee na kwa wateja wa StarTimes wanatakiwa kulipia kifurushi cha MAMBO kwa Tsh 14,000 kwa upande wa Antenna na wale wanaotumia dish watalipia Tsh 21,000 tu, kupata uhondo huu.
Mbali na ligi ya EUROPA StarTimes wanaonyesha ligi ya Bundesliga pamoja ile ya Ufaransa, maarufu kama Ligue 1. Katika Bundesliga wikiendi hii kuna mchezo mkubwa ambao unafahamika kama Der Klassiker unaokutanisha miamba miwili, wazee njano na nyeusi Borussia Dortmund watawakaribisha Bayern Munich katika dimba la Signal Iduna Park saa 2:30 Usiku jumamosi hii.
Dortmund ndio vinara wa ligi hiyo baada ya kuanza vizuri msimu huu wakiwa hawajapoteza mchezo wowote hadi sasa. Bayern ambao wamesuasua sana msimu watakuwa na kibarua kigumu kuidhibiti safu ya ushambuliaji ya Dortmund ambayo in amagoli kila kona.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...