Kwa mara ya tatu mfululizo, CITI Foundation ikishirikiana na Shirikisho la Asasi zinazotoa huduma ndogo za fedha (TAMFI), jana wamezindua awamu ya tatu ya tuzo za wajasiriamali za CITI (CITI Micro entrepreneurship Awards – CMA).
Tuzo hizi zinalenga kutambua mchango mkubwa wa wajasiriamali kwenye kuinua uchumi wa familia zao na jamii zinazowazunguka.
Kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa Citibank Tanzania, Bw. Joseph Carasso, tuzo za CITI zimeshamiri na katika kipindi cha miaka miwili iliyopita kumekuwa na mafanikio makubwa kwa wajasiriamali wadogo na walio wabunifu.
Mtendaji huyo alisema CITI inaamini kuwa wajasiriamali wadogo wenye ubunifu ndio wajasiriamali wakubwa wa kesho. Tunawathamini sana.
Tuzo za wajasiriamali za CITI (CMA) zimekuwa alama kubwa ya utendaji wa kazi za Citi Foundation kwa zaidi ya muongo mmoja.
Tangu mwaka 2005, wakati zilipoanzishwa nchini Marekani tuzo za CITI, zimelenga kuleta mageuzi ya kiuchumi na fursa kwa wajasiriamali katika nchi zaidi ya nchi thelatini duniani kote.
Mtendaji mkuu Citi bank Tanzania joseph Carasso akizungumza. Mwingine ni wmenyekiti wa bodi ya Tamsi Joel Mwakitalu.
Washiriki katika uzinduzi
Mtendaji wa TAMFI Terry akielezea hafla  ya uzinduzi wa tuzo.
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...