Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme nchini (Tanesco) Dkt Alexander Kyaruzi  katika akiwa kwenye picha ya pamoja kulia kwake ni Mjumbe wa bodi ya Shirika hilo Balozi James Nzagi  na kushoto ni kwake ni Mjumbe wa Bodi hiyo Gilay Shamika

Bodi yaWakurugenziya TANESCO imesema inaridhishwa na Ubora wa mita zinazozalishwa hapa nchini kwani zinaviwango sawan amita zinazo zalishwa njeya nchi.

Hayo yalibainishwa leo wakati wa ziara iliyofanywa na Bodi yaWakurugenzi hiyo katika kiwanda cha Inhemeterna Baobab Energy System vilivyopo mjini Dar es salaam, Mwenyekiti wa Bodi yaWakurugenziya TANESCO Dkt. Alexander Kyaruzi amesema kuwa dhumuni kubwa la ziara hiyo ni kukagua na kujiridhisha na ubora wa mita na uwezo wa viwanda hivyo katika kukidhi mahitaji ya TANESCO na REA.

Alisema kwani kwasasa uhitaji wa Mita umekua mkubwa kutokana na uhitaji wa umeme kwa wananchi wa Vijijini na Mjini, pamoja na maboresho yanayofanywa na Shirika yakubadilisha mita za wateja wa zamani ambao walifungiwa mita miaka 10 iliyopita na sasa wanahitajika kuwekewa mita mpya.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme nchini (Tanesco) Alexander Kyaruzi kulia akiangalia mchakato wa utengenezaji wa mita katikati ni Meneja Mwandamizi wa Usambazaji na huduma kwa wateja wa shirika hilo Theodory Bayona  na kushoto ni Mkurugenzi wa Kiwanda cha cha Inhemeter
 Mkurugenzi wa Kiwanda cha cha Inhemeter kushoto akisisitiza jambo kwa  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme nchini (Tanesco) Alexander Kyaruzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...