Na Grace Semfuko-MAELEZO.
Bunge la Jamhuri ya Watu wa China
limepongeza kasi ya ujenzi wa Miradi inayofanywa na Serikali ya
Tanzania na kwamba ushirikiano uliopo baina ya China na Tanzania
utaendelea kuimarishwa ili kuzifanya nchi hizo kuzidi kuwa na maendeleo
ya kuichumi
Hayo yamebainishwa na Makamu wa
Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya watu wa China Bw. Cai Defang
alipotembelea Darala la Nyerere Kigamboni Jijini Dar Es Salaam
lililojengwa na Kampuni ya China Railway Jiangchang Engineering CRJE na
China Major Bridge Engineering Company ujenzi ulioanza mwaka 2012 na
kukamilika April 2016.
Daraja hilo linalovuka mkondo wa
maji wa Kurasini hadi Kigamboni Jijini Dar Es Salaam lina urefu wa mita
680 na njia sita za kupitishia magari ni daraja kubwa katika nchi za
Afrika Mashariki na lilizinduliwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli April
19 mwaka 2016 na kupewa jina la Julius Nyerere kwa heshima ya Rais wa
Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere.
Ujenzi wa Daraja la Nyerere
ulibuniwa na Serikali lengo likiwa ni kupunguza msongamano wa magari
uliokuwepo katika kivuko cha Magogoni Jijini Dar Es Salaam na
kurahisisha usafiri lengo ni kuwaondolea watanzania changamoto kwenye
sekta ya usafirishaji.Akizungumza katika ziara hiyo
Makamu Mwenyekiti huyo wa Bunge la Jamhuri ya Watu wa China Cai Defang
amesema ni muda muafaka sasa kwa daraja hilo kutumika kama njia za
kiuchumi kwa watu wa Tanzania.
Makamu wa Rais wa Bunge la Jamhuri ya Watu wa China Mhe. CAI Dafenga akipunga mkono wakati alipotambulishwa Bungeni mapema leo Jijini Dodoma. Wa pili toka kulia ni Naibu Spika wa Bunge Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Balozi wa China nchini Bi. WANG wa kwanza kulia. Makamu huyo wa Rais ametembelea Bunge la Tanzania akiambatana na Wabunge kumi na tano kwa lengo la kudumisha ushirikiano baina ya pande zote mbili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...