SHIRIKA la utu wa mtoto nchini (CDF) limesaini makubaliano na ubalozi wa Nertheland nchini ambayo imetoa jumla ya shilingi milioni 60 zilizolenga kupunguza vitendo dhidi ya watoto na wanawake.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi mtendaji wa CDF Koshuma Mtengeti amesema kuwa Netherland wamekuwa marafiki wazuri katika kuhakikisha wanawake na watoto wanaishi huru na hiyo ni kwa kutoa msaada ambayo inasaidia kupinga vitendo hivyo vya ukatili.

Mtengeti amesema kuwa fedha hizo zitatumika katika programu jijini Dodoma katika Wilaya ya Mpwapwa na hiyo ni kutokana na hali ya juu ya ukatili jijini humo.Aidha amesema kuwa maeneo yatakayoangaliwa ni pamoja na kujua vyanzo vya matukio hayo, jinsi ya kufanya kazi na kamati ya kutokomeza matukio hayo na kuwajengea watoto na wanawake uwezo wa kutoa taarifa kuhusiana na matukio hayo.

Aidha amesema kuwa maeneo yatakayoangaliwa ni pamoja na kushirikiana na jeshi la polisi, wanajamii katika kulinda haki za watoto na wanawake pamoja na wanaume katika kushiriki katika kulinda haki na kutoa taarifa dhidi ya vitendo vya ukatili.

Pia amesema kuwa programu hiyo ni kubwa na wamefanya katika makao makuuu ya nchi ili kuweza kutoa taarifa sahihi kwa serikali ili kuweza kupunguza asilimia 40 za ukatili kwa wanawake.

Kwa upande wa balozi wa Netherlands nchini Jeroen Verheul amesema kuwa wanashiriki katika programu hizo ili kuhakikisha haki za wanawake nchini zinalindwa na wanafurahi kufanya kazi na shirika hilo na wana imani malengo ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake yatapungua kwa kiasi kikubwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...