Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema Novemba 23.2018 itatoa uamuzi wa kumfutia dhamana ama la Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini Ester Matiko baada ya wiki iliyopita kutoa amri ya kukamatwa kwa washtakiwa hao kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

Hatua hiyo imekuja baada ya watuhumiwa hao kufika mahakamani wenyewe na kujieleza.

Akitoa maelezo yake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, Mbowe amedai kuwa anaiheshimu mahakama sana na anatambua kama kiongozi na kama raia nafasi ya Mahakama katika kusimamia haki kwenye taifa.

Amesema, ni ukweli usiopingika kuwa yeye na washtakiwa wenzake ni viongozi na wana majukumu mengi ya kiungozi ya kutendaji ndani na nje ya nchi.

Mbowe ameeleza kuwa Oktoba 28, alisafiri kwenda Washington DC kwenye mkutano wa Oktoba 30, mwaka huu na kwamba kwa ratiba yake alistahili kuondoka huko Oktoba 30, usiku na kurejea Dar es Salaam Oktoba 31 kwa ajili ya kuendelea na Kesi Novemba Mosi, mwaka huu lakini bahati mbaya kabla hajaanza safari hiyo alipata matatizo ya ugonjwa ambapo kwa mazingira aliyokuwepo haikumruhusu kusafiri safari ndefu ya ndege kwa ushauri wa kitabibu na miiko ya kinachomsumbua.

Ameongeza, katika jitihada za kujaribu kupata Matibabu nchini Marekani zilikwamishwa na bima yake ya Matibabu ya kimataifa kwa sababu nilikuwa ikimruhusu kutibiwa katika nchi ambazo siyo Marekani wala ulaya bali inaruhusu atibiwe kati nchi za Afrika mashariki, Afrika Kusini na Dubai.

Amedai kufuatia hivyo, ilimlazimu kutafuta miadi kwenda kwenye Matibabu katika nchi za Emirate na kwamba hiyo ni kutokana na ushauri aliopewa mbali na bima, kutokana na utofauti wa Masaa kati ya matano iwapo atatoka alipo kwenda Dubai kwamatibabu na ni zaidi ya 24 iwapo angekuwa nchini.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...