Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Desemba 18 mwaka huu inatarajia kutoa hukumu dhidi ya kesi ya matumizi mabaya ya madaraka inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando.

Katika kesi hiyo, Tido anakabiliwa na mashtaka manne ya kutumia madaraka vibaya na moja la kuisababishia Serikali hasara ya Sh.milioni 887.1.

Hakimu Mkazi Mkuu,Huruma Shaidi anayesikiliza kesi hiyo, amefikia hatua hiyo baada ya Wakili wa Serikali kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa( Takukuru), Leonard Swai kuieleza Mahakama kuwa wamekwisha wasilisha majumuisho yao ya mwisho mahakamani hapo.

Naye Wakili wa utetezi wa Tido, Dk. Ramadhani Maleta ameiarifu Mahakama kuwa wakili mwenzake Martin Matunda ambaye walikuwa na wakimtetea Tido, amefariki dunia na lakini nao pia wamekwisha wasilisha hoja zao za mwisho.

Kutokana na taarifa hiyo Swai ameiomba Mahakama kuipangia Kesi hiyo tarehe ya hukumu ambapo Hakimu Shaidi amepanga kusoma hukumu hiyo Desemba 18, mwaka huu.Mwishoni mwa mwezi uliopita, Tido kupitia mawakili wake Martin Matunda na Dk Ramadhani Maleta walifunga ushahidi wa upande wa utetezi.

Katika kesi hiyo jumla ya mashahidi watatu wa upande wa mashtaka katika kesi hiyo walitoa ushahidi na kufunga ushahidi wa upande wa mashtaka.Miongoni mwa mashahidi hao ni Afisa uchunguzi wa Takukuru, Victor Lesuya, Mwanasheria wa TBC, Gwakisa Mlawa na Mkurugenzi Mkuu mstaafu wa TBC, Clement Mshana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...