Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii .

CHAMA cha Waajiri Tanzania (ATE) wamefanya mkutano mkuu wa kwanza wa wanawake katika uongozi kwa mwaka 2018 uliombatanisha mahafali ya pili ya programu ya mwanamke wa wakati ujao (Female Future Programme). 

ATE wamefanya mkutano huo wakishirikiana na Shirikisho la vyama vya waajiri nchini Norway (NHO) wenye lengo la kuwajengea uwezo wanawake kwa ajili ya kushika nafasi za juu za uongozi na kuwapa uwezo wa kuingia kwenye bodi mbalimbali na kushiriki katika maamuzi. 

Akifungua Mkutano huo, Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira ma Wwtu wenye Ulemavu Jenista Mhagama amesema mkutano huu mkubwa wa mwaka wa uongozi kwa wanawake unaenda samamba kabisa na juhudi za nchi yetu katika kuhakikisha idadi ya wanwake kwenye nafasi zao za juu za uongozi inazidi kuongezeka pia wanawake kuwa na idadi kubwa ya uwakilishi katika bodi za wakurugenzi za makampuni mbalimbali. 

"Serikali ya awamu ya tano imeendelea kusimamia na kuhakikisha kunakuwa na uwiano mzuri wa viongozi wanawake ndani ya serikali na jumuiya mbalimbali , makampuni ya kibiashara nchni na katika kufanikisha hili serikali imeanzisha mpango mkakati wa kitaifa kwa ajii ya maendeleo ya usawa wa kijinsia ambapo upo kwenye dira ya maendeleo ya Taifa 2025"amesema Jenista. 

Jenista amesema, programu hiyo ni fursa kwa wanawake wa wakati nujao na mafunzo hayo wakiyatumia vizuri yatawasaidia kuendesha maisha katika nyanja mbalimbali, kazini, nyumbani, kwenye jamii na kwa kizazi kijacho. 

Amesema, kwa mwaka 2017 idadi ya wanawake katika bodi mbalimbali za taasisi za serikali iliongezeka na kufikia 117 kutoka 114 kwa mwaka 2014 ikilinganishwa na wanaume ambapo walipungua toka 526 mwaka 2014 hadi 352 mwaka 2017, aidha katika miaka hiyo idadi ya wanawake majaji imeongezeka na kufikia 39 kati ya majaji 95, wakati mwaka 2012 majaji wanawake walikuwa 34 kati ya 97. 
Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira ma Wwtu wenye Ulemavu Jenista Mhagama akizunguzma wakati wa mkutano mkuu wa kwanza wa wanawake katika uongozi kwa mwaka 2018 uliombatanisha mahafali ya pili ya programu ya mwanamke wa wakati ujao (Female Future Programme).
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waajiri Nchini (ATE) Dkt Aggrey Mlimuka akizzungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano mkuu wa kwanza wa wanawake katika uongozi kwa mwaka 2018 uliombatanisha mahafali ya pili ya programu ya mwanamke wa wakati ujao (Female Future Programme). 
Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira ma Wwtu wenye Ulemavu Jenista Mhagama akitoa cheti kwa moja ya wahitimu Arafa wakati mkutano mkuu wa kwanza wa wanawake katika uongozi kwa mwaka 2018 uliombatanisha mahafali ya pili ya programu ya mwanamke wa wakati ujao (Female Future Programme). 
Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira ma Wwtu wenye Ulemavu Jenista Mhagama akitoa cheti kwa moja ya wahitimu Bahati Minja wakati mkutano mkuu wa kwanza wa wanawake katika uongozi kwa mwaka 2018 uliombatanisha mahafali ya pili ya programu ya mwanamke wa wakati ujao (Female Future Programme).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...