Na. Vero Ignatus, Arumeru. 

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro amejitolea kuwasadia kuandika Maandiko ya kibiashara wananchi wanaotaka kufanya Kilimo na Ufugaji wa Kibiashara ili waweze kukopesheka na Ta asisi za kifedha 

Amesema hatua hiyo imefikia baada ya kubaini kuwepo kwa vikwazo katika maandiko katika hatua za awali kwani Taasisi hizo kabla ya kutoa msaada au mkopo huitaji mchanganuo, andiko la kibiashara kwanza kabla ya kuwawezesha wananchi ambao wanataka kuanza kilimo au ufugaji wa kibiashara.

Wanapoanza safari ya kutimiza ndoto zao za kuwekeza katika sekta hizo, ambapo baada ya kubaini uwepo wa vikwazo hivyo aliamua kujiongeza Kwa kutafuta wadau ambao atashirikiana nao katika kuwasaidia wananchi kuondoa Vikwazo hivyo.

Mhe Muro amesema tayari kampuni Binafsi ya Wawezeshaji wa wakulima (PASS)Private Agricultural Sector Support imekubali kuwaandalia na kugharamia Mpango kazi wa kibiashara zitakazowasaidia Wakulima na Wafugaji katika kupata Mkopo katika Taasisi za Kifedha hali ambayo itawasaidia katika uendelezaji wa Kilimo chenye tija na ufugaji wa kibiashara. 
 Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro akipata maelezo ya bidhaa kutoka kwa mmoja wa mkulima katika maonyesho ya wakulima wilayani hapo. 
DC Muro akizungumza na wakulima katika maonyesho hayo ya kilimo yaliyoanza tarehe 1-3 Novemba 2018 wilayani humo. 
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro akizungumza na wakulima na wananchi wa wilaya hiyo katika maonyesho hayo ya wakulima
Mmoja kati ya mkulima. Wilayani humo akimpatia maeleza ya mbegu ya mahindi kama inavyoonekana katika picha Mkuu wa wilaya Jerry Muro katika maonyesho hayo
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro akiwa katika picha ya pamoja na wakulima katika maonyesho hayo ya wakulima Meru. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...