Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii Newala, Mtwara

Mkuu wa Wilaya ya Newala Aziza Mangosongo leo amepokea ujumbe wa Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ )ambao umeanza kukagua Maghala yote ya kuhifazia korosho katika Wilaya hiyo kama ilivyoagizawa na Rais John Pombe Magufuli kufuatia Wafanyabiashara kutaka kuwalangua wakulima kwa kununua kwa bei isiyokuwa na Maslahi.

Ujumbe huo ambao ulipata nafasi ya kutembelea Maghala yote Makubwa ambayo yapo katika Wilaya yake hili waweze kuanza zoezi la kununua korosho kwa kuwalipa wananchi kupitia benki ya kilimo.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Newala mkoani Mtwara, Daniel Zenda amesema sababu kubwa ya kupungua kwa uzalishaji wa zao la korosho msimu huu ni kutokana na mvua iliyonyesha katikati ya msimu na kusababisha dawa ya Sulpher kushindwa kufanya kazi vizuri.

Akitoa muhtasari kwa vyombo vya habari jana mjini Newala juu ya shughuli zilizofanyika hadi sasa tangu serikali kutoa mwongozo wa ununuzi wa korosho, Zenda alisema propaganda zinaoenezwa kuwa upungufu wa uzalishaji umetokana na wakulima kutokupewa fedha za ushuru wa kusafirisha nje ( export levy) hazina ukweli wowote.

"Upungufu wa uzalishaji wa korosho haujasababishwa na kukosekana kwa fedha za export levy kama inavyoelezwa na baadhi ya wanasiasa badala yake mavuno yamepungua kwasababu mvua zilinyesha katikati ya msimu na kusababisha athari kwa dawa ya sulpher kushindwa kufanya kazi vizuri kwenye mazingira hayo," alisema Zenda.

Mkuu wa Wilaya ya Newala AkiongozaUjumbe wa Kikosi cha Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Ambao wamefika Wilayani hapo kwa ajili ya kukagua Maghal ya Korosho hili waanze zoezi la ununuzi na kulipa fedha kwa wakulima kama ilivyoagizwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr . John Magufuli kuwa Korosho zote zitanunuliwa na jeshi .
Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakiwa ndani ya Ghala la Kiwanda cha Ubanguaji wa korosho Microfonix kilichopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara
Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakiwa ndani ya Ghala la Agro focus kilichopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara
Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakiwa ndani ya Kiwanda cha Ubanguaji wa korosho Microfonix kilichopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara na kushuhudia zoezi la usafishaji wa korosho.
Wafanyakazi wa Kiwanda cha Ubanguaji wa Korosho cha Microfonix wakiendelea na kazi ya ubanguaji wa korosho na kusafisha katika Kiwanda hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...