*Asema inasikitisha watumishi wa umma kupoteza maisha kwa ajali
*Awataka waache kukimbia mwendo kasi, kupita magari bila uangalifu

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

KAMANDA wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Fortunas Muslimu ametoa onyo kali kwa madereva wa Serikali ambao hawazingatii sheria za usalama barabarani na kusababisha ajali zinazokatiza maisha watumishi wa umma ambao Serikali imetumia fedha nyingi kuwaandaa huku akisisitiza atakayevunja sheria atamnyakua tu na sheria kuchukua mkondo wake.

Amesisitiza umuhimu kwa madereva wote nchini wakiwamo hao wa Serikali kuhakikisha wanatii sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali ambazo zinaepuka iwapo sheria zitazingatiwa. Kamanda Muslim ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati anazungumza na Michuzi Blog iliyotaka kupata kauli yake kutokana na kuibuka kwa ajali za barabarani ambazo nyingi zinahusisha magari ya Serikali ambapo amesema jambo la msingi ni kuhakikisha madereva wanatii sheria zilizopo.

"Tumedhamiria kuchukua hatua kwa madereva wote wa Serikali wanaoshindwa kuheshimu sheria za usalama barabarani na matokeo yake kusababisha ajali ambazo kimsingi zinaepukika.Madereva wote wa Serikali wote wamekwenda chuo na wanajua vema sheria za usalama barabarani.Hivyo hizi ajali ambazo zinatokea kwangu naona ni maksudi na wala hakuna sababu nyingine zozote zenye mashiko.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...