*Wateja milioni 1 na wakala 40,000 kupata huduma ya malipo ya Visa kupitia Halopesa. 

Kampuni ya Teknolojia ya malipo ya kimataifa ya VISA imetangaza ushirikiano wa mkakati na Halotel ili kuwezesha malipo ya Visa kwenye simu kwa kutuma codi ya QR kwa wateja wa Halotel nchini Tanzania. 

Huduma hiyo itakayotolewa mwanzoni mwa mwaka 2019 na hivyo kuwezesha wateja zaidi ya milioni moja wa HaloPesa kutumia Visa kwenye simu ili waweze kufanya malipo ya biashara kwa salama na kuweka na kutoa fedha kwa mawakala wa Visa.Mteja yoyote wa HaloPesa, ikiwa ni pamoja na wale ambao hawana akaunti ya benki, wataweza kufaidika na huduma hii. 

Lengo la huduma hii ni kuunganisha Watanzania zaidi kwenye mfumo wa malipo ya kimataifa, kuleta huduma ya malipo ya Visa ya usalama na urahisi kwa watumiaji na wafanyabiashara. 

"Tunafurahia ushirikiano huu na mojawapo wa kampuni maarufu ya simu ya Halotel, Ushirikiano wetu na Halotel utahakikisha kuwa Watanzania wanaweza kufanaya malipo ya QR kwa kutumia Visa kwenye simu zao kwa wauzaji na wafanyabiashara zaidi ya 40,000. Pia itasaidia kuongeza ushirikishaji wa kifedha kwa watumiaji ambao sasa wataweza kufaidika na kushiriki katika mfumo wa eco Visa ", alisema Meneja Mkuu wa Visa wa Afrika Mashariki, Kevin Langley. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...