Kumekucha Kwenye Promosheni ya Shinda Zaidi na SportPesa maana watanzania wanazidi kushinda bajaj kutokana na ubashiri wanaofanya kupitia timu ya ushindi.

Safari hii kambi ya timu ya ushindi imehamia hapa jijini Dar es salaam katika viunga vya Mbezi Juu ambapo kuna mshindi wa droo ya 57 Emmanuel Nzuki anayekabidhiwa bajaj baada ya ushindi.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa bajaj hiyo Nzuki alisema hakuamini kama anaweza kushinda maana mara kadhaa alikuwa anacheza mara nyingi lakini hakubahatika kumbe wakati wake ulikuwa haujafika kubahatika sasa ndio ameamini baada ya kuupokea ushindi huo

"Ama kweli nimeamini bahati ya mtu haipotei unajua vile nilikuwa nikiona wengine wakishinda nilijua labda wanaoshinda ni wale wenye kipato cha chini kabisa kumbe hata sisi wenye kipato cha kati inawezekana, siku ya leo yote naitumia kusherekea ushindi wangu" alisema Nzuki.

Aidha mshindi huyo aliongeza kuwa bajaj hiyo itaweza msaidia kuinua kipato chake na kuacha maisha ya kutegemea mshahara pekee. "Sikia nikwambie aisee ni kweli nina mshahara mzuri lakini bado bajaj hii itakuwa msaada mkubwa kwangu maisha ya kutegemea mshahara pekee ni magumu sana lakini kupitia bajaj hii naweza sasa boresha maeneo mengine mfano kulipia watoto wangu ada ya shule kuwasaidia ndugu na pesa nyingine naweza malizia malipo ya kiwanja changu na kuanza kujenga.

 Mshindi wa droo ya 57 Emmanuel Nzuki aliyekabidhiwa bajaj baada ya ushindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...