NA TTGANYA VINCENT,RS TABORA

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imeamua kuweka ulinzi katika shule za Msingi za Manispaa ya Tabora nyakati za masomo ili kuzuia kusije kukatolekea kwa vitendo vyovyote vya kuwazulu na kuwateka wawapo shuleni.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kufuatia vurugu kubwa zilizotokea leo katika Shule ya Msingi Chemuchemu baada ya kuwepo kwa hisia ya watoto wawili kutekwa.

Alisema hadi hivi sasa hajajulikana kama kweli kuna watoto wa Shule hiyo waliotekwa na kupandishwa katika gari aina ya Noah.Mwanri alisema wamejaribu kufuatilia ili kujua ni watoto gani na majina yao ya watoto waliotekwa hakuyapata na wala hakuna mzazi aliyejitokeza kusema kuwa mtoto wake amepotea.

Alitoa wito kama kuna wazazi ambapo watoto wao wametekwa watoe taarifa kwa Polisi au katika Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa ili hatua ziweze kuchukuliwa ikiwemo kuwatafuta.“Kuanzia sasa nimeagiza Polisi kuongeza Doria katika maeneo ya shule za Msingi ili kuwaondolea hofu wazazi…na kama mtu asifahamika ataonekana maeneo ya shule achukuliwe hatua” alisema.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema vurugu hizo zilitokana na wananchi kuwa bado na kumbukumbu ya wiki iliyopita ambapo mtoto wa miaka 6 alitekwa na kuwawa katika eneo la Tambuka Reli.Alisema Jeshi la Polisi linaendelea kulifanyia uchunguzi matukio yote na kuwataka wazazi kuwa watulivu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...