Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

TAASISI isiyo ya kiserikali ya SADAKA Network imeunga mkono juhudi za Hospitali ya Aga Khan, Muhimbili na Taasisi ya Women to Women katika kufanikisha upasuaji wa urekebishaji (upasuaji wa urembo) kwa wanawake na watoto utakaofanyika 27 November mwaka huu. 

Hospitali ya Agha Khan, Muhimbili na Taaisis ya Women to Women ziko kwenye harakati za kuweka tabasamu kwenye nyuso za wahanga wa ukatili wa nymbani uliosababisha wahanga hao kuathirika. 

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Mwanzilishi wa SADAKA Network Dkt Ibrahim Msengi amesema kuwa SADAKA Network umeamua kuunga mkono kwa kuchangisha fedha kupitia programu yake ili kufanikisha mpango huo, wameamua kutumia viongozi wa jamii na watu maarufu ndani ya Tanzania kuhabarisha wananchi wote ili waweze kuchangisha fedha ili kwa pamoja waweze kusaidia kurejesha tabasamu kwenye uso zao. 

Dkt Ibrahim amesema kuwa, ukatili wa nyumbani na ajali unaweza ukasababisha mauti au majeraha yanayoweza kubadilisha muelekeo wa maisha ya yao, watu wameshuhudia, kusikia au kuona kupitia luninga wanawake na watoto ambao muonekano wao umebadilika kisa ajali au ukatili wa nyumbani au watoto wenye maisha yaliybadilishwa kisa wazazi waliowakatili. 
Mwanzilishi wa SADAKA Network Dkt Ibrahim Msengi akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na taasisi yake kuunga mkono juhudi za Hospitali ya Aga Khan, Muhimbili na Taasisi ya Women to Women katika kufanikisha upasuaji wa urekebishaji (upasuaji wa urembo) kwa wanawake na watoto utakaofanyika 27 November mwaka huu, kushoto ni Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum na Meneja Masoko na Mahusiano wa Agha Khan Hospital Olayce Steven Lotha .
Meneja Masoko na Mahusiano wa Agha Khan Hospital Olayce Steven Lotha akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na upasuaji wa urekebishaji (upasuaji wa urembo) kwa wanawake na watoto utakaofanyika 27 November mwaka huu. 
Balozi wa Rejesha tabasamu usoni mwao Yvyone Cherry akiwa anawahisi jamii kuchangia kwa kiasi chochote ili kufanikisha upasuaji wa wanawake na watoto waliofanyika ukatili majumbani. Kushoto ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Jackson Jackson, Mwanzilishi wa SADAKA Network Dkt Ibrahim Msengi na Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum. 
Waandishi wa habari na wadau mbalimbali wakifuatilia mkutano huo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...