Na.Alex Sonna wa Fullshangweblog,Dodoma
Mfuko
wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Jijini
Dodoma,wametakiwa kutilia mkazo ulipaji wa mafao ya wastaafu kwa wakati.
Akitoa
maagizo hayo leo jijini hapa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,
Ajira na Vijana na Wenyeulemavu, Anthony Mavunde, alipotembelea ofisi za
mfuko huo kusikiliza maoni ya wanachama na wadau wanaohudumiwa na
PSSSF.
Mhe.Mavunde
amesema kuwa inatakiwa mlipe kwa wakati mafao kama ilivyo kauli mbiu
yenu ya “Tunalipa Kuanzia jana” ili lengo la serikali la kuunganisha
mifuko ya hifadhi ya jamii, litimie .''Inatakiwa
wastaafu wapewe umuhimu wa elimu kabla ya kuwalipa mafao ili waweze
kujiandaa vyema kwa kuanzisha miradi na kutunza kumbukumbu za matumizi
ya fedha''amesema Mavunde
Aidha
Mhe.Mavunde amewaagiza wafanyakazi wote kuhakikisha wanatoa huduma
stahiki zenye ubora na kwa wakati ili kuisaidia serikali kusonga mbele
katika huduma ya hifadhi ya jamii.“Matarajio
ni kwamba mtatoa huduma kwa ufanisi na kwa ubora ili yale matarajio ya
serikali yaweze kutimia, awali kulikuwa na malalamiko watu hawapati
huduma stahiki lakini naimani hakutakuwa na malalamiko hayo,”amesema
Mavunde
Kwa
Upande wake, Meneja wa PSSSF Mkoa wa Dodoma, Meshack Bandawe, amesema
kuwa ofisi hiyo imeanza kufanya kazi zake Septemba mosi mwaka huu na
kuna wanachama wanaochangia ni zaidi ya laki moja.“Tumejipanga
kuwahudumia ipasavyo na hadi sasa tumekusanya Sh.Milioni 880 katika
mkoa wa Dodoma na tutaendelea kusimamia na kutekeleza majukumu kwa
mujibu wa sheria,”amesema Bandawe
Hata
hivyo amebainisha kuwa hadi sasa wanachama 2792 wameshapita kupata
huduma na wamepokea madai 796 ya wanachama wa mifuko mbalimbali
iliyounganishwa kwenye mfuko huo. Bandawe
amesema kuwa madai 717 yameshughulikiwa na wanachama wamelipwa mafao
yao na mengine 79 yapo kwenye hatua mbalimbali za kufanyiwa kazi katika
mkoa wa Dodoma tu.
Aidha
amesema takribani wastaafu 1027 wanatarajiwa kustaafu katika kipindi
cha 2018/19 ambapo mfuko huo umejipanga kutoa elimu ya kujipanga na
ustaafu wao ikiwemo kubuni miradi ya kujiimarisha kiuchumi kwa mkoa wa
Dodoma peke yake.
Naibu
Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Vijana na Wenyeulemavu,
Anthony Mavunde,akizungumza waandishi wa habari (hawapo pichani)
alipotembelea ofisi za mfuko huo leo jijini Dodoma kusikiliza maoni ya
wanachama na wadau wanaohudumiwa na PSSSF.
Naibu
Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Vijana na Wenyeulemavu,
Anthony Mavunde,akizungumza na Meneja wa PSSSF Mkoa wa Dodoma, Meshack
Bandawe, alipotembelea ofisi za mfuko huo kusikiliza maoni ya wanachama
na wadau wanaohudumiwa na PSSSF.
Naibu
Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Vijana na Wenyeulemavu,
Anthony Mavunde,akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa PSSSF
Mkoa wa Dodoma leo alipotembelea ofisi za mfuko huo kusikiliza maoni ya
wanachama na wadau wanaohudumiwa na PSSSF.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...