Na Amiri Kilagalila ,Njombe 

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) mkoani Njombe inawashikilia watumishi watano wa Halmashauri ya Makete akiwemo Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Francis Namaumbo kwa ubadhirifu mkubwa wa fedha zaidi ya Sh.milioni 500.

Akizungumza leo Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Njombe Chalse Nakembetwa amesema kuwa upotevu wa fedha hizo umetoka katika makusanyo ya Julaihadi Semptemba ambapo yalikuwa ni zaidi ya Sh.bilioni moja huku taarifa zikionesha kuwa zaidi ya Sh.milioni 500 zimepotea na wahusika wakishindwa kutoa maelezo ya kutosha baada ya kuhojiwa na taasisi hiyo.

Amesema katika uchunguzi Takukuru imebaini wizi na ufisadi unaofanywa na baadhi ya watendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Makete zaidi ya Sh.milioni 5.69 sawa na asilimia 46 zilizokusanywa kwa utaratibu wa POS kwa kipindi cha Julai hadi Septemba 2018 hazijulikani zilipo.

Amefafanua makusanyo hayo yalikuwa ni sehemu ya Sh.1,245,632,633 yaliyokusanywa katika kipindi tajwa .Kutokana na uchunguzi huo Takukuru Mkoa wa Njombe inawashikiria baadhi viongozi na watendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Makete kwa ajili ya uchunguzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...