Tarehe hii mwaka jana, alfajiri alipoamka;
mawili akaongea, usingizini kurejea;
tukaita hakuitika; kumbe amehitimisha,
kwa kauli na vitendo, aliposema: “naba ndioo”,
kama anayetwambia kazi ameimaliza, 
kwamba saa ilishatimia, atavuka kwenda ng’ambo tupokee kishujaa. 
Mama amefaulu, hatulii, twashangilia.


Amebaki shujaa wetu kama Baba alivyokuwa.
Kushughulika na kuelekeza, mahitaji ya wanae kama Mwalimu stadi awezavyo darasa. 
Kila mwanae alijisikia amefika na kujiona muhimu kwake,
naye akawa rubani, kutuongoza safarini;
Akatujengea umoja, utuongozao mpaka kesho.
Ukidhihirika kwa jamaa pana, ya waume wa binti zake na wake wa wanae, 
watoto na wajukuu, vitukuu na vilembwe. 
Ukali twaukumbuka, alishikilia nidhamu,
hakutaka tupotee, kiimani, mila na desturi.
Alisimamia elimu na kuhimiza bidii, hakuwa na mzaha akisema waziwazi: 
afadhali msumbuke sasa faida mtaiona baadaye.
Aliiishi nidhamu, akawa mfano kwetu na wajao nyuma yetu.
Ya kwamba maisha bora ni bidii, kutokukata tamaa na kumtegemea Mungu.
Tunaposheherekea mwaka mmoja, twakumbuka ukarimu wake, 
Waliomtembelea hawakuondoka, bila chai, chakula na heri kuwaombea
Alithamini mila na desturi 
Akajiunga na kina mama, vyamani kijijini na mjini; 
Marafiki rika mbalimbali akawagusa watu wengi;
Alikuwa na elimu  
kuhimili changamoto,kujadili na wenye elimu mbalimbali bila kubaki nyuma
kipaji chake cha kumbukumbu kilikuwa kitabu cha historia, kilichoandikwa kwa umakini 
kukumbuka yaliyojiri, kwa habari za kijamii za furaha na huzuni, 
kwa habari za koo, za mila na desturi
Tunamshukuru Mungu tukisherehekea maisha yake. Alivipigana vita vizuri mwendo akaumaliza na imani akailinda.
Atakumbukwa daima na watoto Rhoda, Regina, Anders, Doris, Melissa, Alison, Aldin, Proscovia na Jovian; Wakwe wake na watoto wa kuwalea, wajukuu na vitukuu, ndugu,jamaa na marafiki,Daima tutamuenzi
Shukurani ya pekee itatolewa katika Kanisa la KKKT/NWD Usharika wa Kabale Bukoba, tarehe 18/11/2018

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...