Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kulia akijadiliana jambo na Meneja wa kampuni ya Kizalendo ya Songoro Marine Boatyard ya jijini Mwanza Major Songoro mara baada ya kukagua kivuko cha MV. Chato ambacho ukarabati wake umemalizika, kivuko hicho chenye uwezo wa kubeba tani 75 sawa na abiria 200,na magari 6 kinatoa huduma Wilaya ya Chato, maeneo ya Ikumba Itale, Izumacheli, Muharamba, Senga, Bukondo na Bwina Mkoani Geita .
 Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle wa pili kulia akisisitiza jambo kwa Meneja wa kampuni ya Kizalendo ya Songoro Marine Boatyard Major Songoro wa pili kushoto mara baada ya kukagua kivuko cha MV. Chato ambacho ukarabati wake umemalizika, tukio lililofanyika katika yadi ya Songoro iliyopo Ilemela mjini Mwanza. Kivuko hicho cha tani 75 kina uwezo wa kubeba abiria 200 na magari 6 na kinatoa huduma katika Wilaya ya Chato, maeneo ya Ikumba Itale, Izumacheli, Muharamba, Senga, Bukondo na Bwina Mkoani Geita. Kushoto ni Mkurugenzi Huduma za Ufundi (WUUM) Mhandisi Lazaro Vazuri na kulia ni Meneja wa TEMESA mkoa wa Mwanza Mhandisi Hassan Karonda.
 Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle (aliyevaa suti) akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua kivuko cha MV. Chato ambacho ukarabati wake umemalizika, tukio lililofanyika katika yadi ya Songoro mjini Ilemela Mwanza. Kivuko hicho cha tani 75 kina uwezo wa kubeba abiria 200 na magari 6 na kinatoa huduma katika Wilaya ya Chato, maeneo ya Ikumba Itale, Izumacheli, Muharamba, Senga, Bukondo na Bwina Mkoani Geita.
 Muonekano wa kivuko cha MV. Chato mara baada ya kukamilika kwa ukarabati wake. Kivuko hicho cha tani 75 kina uwezo wa kubeba abiria 200 na magari 6 kinatarajiwa kurudishwa katika kituo chake kuendelea na kazi ya kuvusha abiria maeneo ya Ikumba Itale, Izumacherl, Muharamba, Senga, Bukondo na Bwina Mkoani Geita.

Kivuko cha MV. Chato kikielea majini baada ya kukamilika kwa ukarabati wake ambao. Kivuko hicho cha tani 75 kina uwezo wa kubeba abiria 200 na magari 6 kinatarajiwa kurudishwa katika kituo chake  Wilayani Chato Mkoani Geita kuendelea na kazi ya kuvusha abiria.
PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO (TEMESA)


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...