Na, Vero Ignatus Arusha
Umoja wa Ulaya (EU) umerithishwa na ujenzi wa maabara ya kisasa ya Tume ya Nguvu za Atomiki (TAEC) ikiwemo uwekaji wa vifaa vyenye thamani ya zaidi ya sh, bilioni 2.3.
Akizungumza mara baada ya kutembelea maabara hiyo, Meneja Mradi na Usalama wa Masuala ya Mionzi, kutoka EU, Genevieve Lizin alisema umoja huo umerithishwa na kazi nzuri ya uwekaji vifaa uliofanywa na serikali.
Alisema Umoja huo umeamua kutoa vifaa hivyo kwaajili ya kudhibiti masuala ya mionzi ndio maana wametoa ili kudhibiti masuala ya mionzi katika nchi za Afrika. "Maabara hii ni ya kisasa na hakuna mfano wake katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla hivyo tumeridhika na kazi waliyofanya Taec katika zoezi la uwekaji vifaa ambavyo sisi tumevitoa "
Mkurugenzi Mkuu Tume ya Nguvu za Atomiki Nchini Profesa Lazaro Busagala akizungumza na Meneja Mredi kutoka Jumuiya ya nchi za Ulaya Genevieve Liz pamoja na wageni wengine alioonhozana nao.
Denis Mwalongo Mkuu wa Idara ya Mionzi, mashine za kuhakiki vifaa vya mionzi katika mwili wa binadamu akiwaonuesha wageni hao kutoka Umoja wa Ulaya jambo
Dkt Wilbroad Muhogora mwenye (shati la draft) Mtafiti wa Tume akifafanua jambo kwa wageni kutoka Umoja wa Ulaya pamoja na, waandishi wa habari
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...