Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James (kulia) akizungumza na Viongozi wa Benki ya CRDB waliofika ofisini kwake leo, kwa lengo la kumtambulisha Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki hiyo, Abdulmajid Nsekela (wa pili kushoto). Ujumbe wa Benki ya CRDB uliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Ally Laay (kushoto), Naibu Mkurugenzi Mtendaji, Esther Kitoka pamoja na Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja, Tully Mwambapa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa tatu kulia) akifafanua jambo wakati wa kikao chao na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James (kushoto) walipomtembela ofisini kwake, jijini Dar es salaam leo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James (wa pili kulia) akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akijadiliana jambo na Naibu Mkurugenzi Mtendaji, Esther Kitoka wakati wa kikao chao na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James.
Picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...