KATIBU Mkuu Kiongozi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Baraza la Taifa la Biashara(TNBC), Balozi John Kijazi amezindua vikundi kazi vya baraza hilo kwa lengo la kujenga na kuimarisha mahusiano kati ya sekta za umma na binafsi katika kuibua changamoto na
kuzijadili kwa mustakabali wa maendeleo ya Tanzania.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa vikundi kazi hivyo jijini Dar es salaam juzi, Balozi Kijazi alisema madhumuni ya kuunda vikundi kazi hivyo vilivyowajumuisha wataalum katika sekta mbalimbali vitawezesha majadiliano juu ya changamoto zajadiliwe kwa kina zaidi kabla ya
kupelekwa katika ngazi ya Baraza.

“jumla ya vikundi kazi vinne nimevizindua leo (juzi) ikiwa ni pamoja na kikundi kazi cha Mazingira ya Biashara, Viwanda, Misitu na Kilimo vitavyokwenda kuibua changamoto na kuleta mapendekezo yatakayosaidia kuboresha sera na miongozo iliyopo,” alisema Balozi Kijazi. Alisema ushirikiano kati ya sekta binafsi na Sekta ya umma unahitajika sana ili kuweza kuibaini changamoto na kuzijadili na kuja na mapendekezo yatakayo leta tija katika mustakabali wa kujenga uchumi wa
Taifa.

“Serikali itapokea mapendekezo yote yatakayowakilishwa na timu za wataalum kutoka katika vikundi kazi hizi na tutayafanyia kazi mapendekezo yote, zaidi kwa mengine yanayoweza kuchukuliwa na maamuzi kwa ngazi yenu endeleeni lengo ni kupunga majadiliano katika ngazi ya
taifa,” alisema Balozi Kijazi Alisisitiza kuwa mijadala ya vikundi kazi hivi ifanyike kwa uhuru na usawa kwa kutoa hofia cheo cha mtu au mali wote wawekitu kimoja ili majadiliano yaweze kuleta tija na mapendekezo yatakayofanya mazingira ya biashara kuboresheka zaidi.
Katibu Mkuu Kiongozi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Baraza la Taifa la Biashara(TNBC) Balozi John Kijazi(kushoto) akisalimia na Kaimu Katibu Mkuu wa TNBC Bi.Oliver Vengula(kulia) mara baada ya kuwasili katika kikao cha uzinduzi wa vikundi kazi vinne vya Baraza hilo jijini Dar es salaam. Wapili kushoto ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania(TPSF) Salum Shamte na wapili kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera na Uratibu, Prof.Faustine Kamuzora
Katibu Mkuu Kiongozi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Baraza la Taifa la Biashara(TNBC) Balozi John Kijazi akizungumza jambo na wajumbe wakamati tendaji wakati wa uzinduzi wa vikundi kazi vinne vya Baraza hilo jijini Dar es salaam zitakavyoleta mapendekezo ya kuboresha sera ,sheria na miongozi ili kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...