Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) imetakiwa kukamilisha kwa wakati mradi wa ujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa cha Kanda ya Ziwa uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza.

Wito huo, umetolewa na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Dorothy Mwaluko wakati wa ziara ya kikazi kuangalia maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho.

Bi. Mwaluko ameitaka Wakala hiyo kuhakikisha inakamilisha ujenzi kwa wakati ili kuiwezesha Serikali kukusanya, kuchambua, kutunza na kuhifadhi kumbukumbu mbalimbali kutoka katika Taasisi za Umma zilizopo kanda ya Ziwa kwa lengo la kulinda urithi andishi na historia ya Taifa letu.

Bi. Mwaluko ameielekeza Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa kuzungumza na Wakala wa Majengo Tanzania na kukubaliana tarehe rasmi ambayo jengo litakuwa limekamilika ili taarifa hiyo itolewe kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa iliyopanga kutembelea kituo hicho hivi karibuni kwa lengo la kujiridhisha na ujenzi uliofanyika.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Dorothy Mwaluko akitazama ramani ya mradi wa ujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Kanda ya Ziwa mkoani Mwanza wakati wa ziara ya kikazi kuangalia maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho. 
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Dorothy Mwaluko akitoa maelekezo ya kuboresha ujenzi wa Kituo cha kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Kanda ya Ziwa mkoani Mwanza kwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) wakati wa ziara ya kikazi kuangalia maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho. 
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Dorothy Mwaluko akizungumza na Wataalam wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) mara baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Kanda ya Ziwa wakati wa ziara ya kikazi kuangalia maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...