Madaktari Bingwa 11 pamoja na wataalam wengine wa afya kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili(MNH) wamewasili katika Hospitali ya Rufaa mkoa wa Lindi Sokoine kwa ajili ya kutoa huduma mbalimbali za afya kwa wananchi wa mkoa huo sanjari na kuwajengea uwezo wataalam wa hospitali hiyo.

Daktari Bingwa wa magonjwa ya kike na uzazi kutoka MNH Geofrey Marandu amesema lengo la ujio wao katika hospitali hiyo ni kuwaongezea ujuzi watalaam wa hospitali za rufaa za mikoa nchini kupitia madaktari bingwa wa Muhimbili lakini pia kupunguza rufaa za wagonjwa kwenda kutibiwa Muhimbili.

‘’Hospitali imeweka mkakati wa kuzitembelea hospitali mbalimbali za rufaa za mikoa nchini ili kushirikiana nao katika kutoa huduma za afya na kuwajengea uwezo , lakini pia kama Muhimbili tunatekeleza agizo la serikali linaloelekeza kupunguza rufaa za wagonjwa kwenda kutibwa nje ya nchi hatua ambayo tayari MNH inaitekeleza hivyo utoaji wa huduma za fya kwa njia ya mkoba utasaidia kupunguza rufaa za wagonjwa kwenda Muhimbili endapo wangepewa rufaa ya kwenda kutibiwa huko’’.amesema Dkt. Marandu.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Sokoine Dkt. Jumanne Shija amesema ujio wa watalaam wa afya wakiwemo Madaktari Bingwa utainufaisha hospitali hiyo kwakua watalaam wake watajengewa uwezo kiutendaji na kupata ujuzi wa kutosha.Ametaja maeneo ambayo wataalam wa hospitali ya Sokoine watanufaika na kujengewa uwezo ni upasuaji, magonjwa ya kike na uzazi, meno, macho, watoto, magonjwa ya mfumo wa mkojo, magonjwa ya koo ,pua na masikio pamoja na masuala ya maabara.

Madaktari Bingwa wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwasili katika Hospitali ya Rufaa mkoa wa Lindi Sokoine kwa ajili ya kutoa huduma za afya na kuwajengea uwezo watalaam wa hospitali hiyo.
Madaktari Bingwa wa MNH pamoja na Madaktari wa Hospitali ya Sokoine wakiwa katika kikao cha asubuhi cha kiutendaji kabla ya kuanza kutoa huduma.
Wauguzi wa hospitali hiyo wakiwa katika kikao cha asubuhi kwa ajili ya kujadiliana masuala mbalimbali ya utoaji huduma za afya.

Daktari Bingwa wa magonjwa ya kike na uzazi Geofrey Marandu akizungumza na mgonjwa ambaye amefika leo katika Hospitali ya Sokoine kwa ajili ya kupata huduma.

Dokta Willybroad Massawe ambaye ni Dkt. wa upasuaji , pua , koo na masiko (kushoto) pamoja na muuguzi Monica Mngoya (kulia) wa Hospitali ya Taifa Muhimbili wakimpatia maelezo mgonjwa ambaye amefika kwa ajili ya kupata huduma za afya.

Baadhi ya wananchi wa mkoa wa Lindi ambao wamejitokeza katika Hospitali ya Rufaa mkoa wa Lindi Sokoine wakisubiri kupatiwa huduma hii leo.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...