Na. Vero Ignatus, Arusha

Mamlaka ya mawasiliano Nchini kanda ya kaskazini imeendesha semina ya siku moja kuhusu huduma za utangazaji kwa chanel zinazotazamwa bila kulipia 

Akizungumza katika semina hiyo Mkuu wa Kanda ya Kaskazini Francis Msungu amesema leo ngo kuu la serikalini kuwataka watoa huduma kujenga miundo mbinu ya Minara hapa nchini na hii itapelekea watanzania wengi watapata ajira. Katika semina hiyo iliyojumuisha viongozi mbalimbali wa serikali ngazi ya mkoa washiriki kuweza kuuliza maswali nje ya mada yanayohudu vifaa vya mawasiliano, simu, tekevisheni pamoja na radio.

Mamlaka hiyo ya Mawasiliano iliweza kutoa ufafanuzi kwamba maduka yanayouza vifaa vya mawasiliano vya eletroniki wauzaji wake wanatakiwa kuwa na leseni kutoka mamlaka ya mawasiliano sambamba na ile ya biashara.Msungu amesema kuwa mafundi wanaotengeneza simu za mkononi wanapaswa pia kwa mujibu wa sheria wawe na kibali kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Nchini.

Ndiyo maana tumeshauri wananchi kupitia viongozi kwamba unapopeleka kutengeneza simu yako kabla hujampa mtu kuitengeneza hakikisha je anacho kibali kinachomruhusu kufanya hiyo shughuli hiyo?
Unapokwenda dukani kununua kifaa chako cha mawasiliano radio, televisheni ni haki yako kujua je huyu anayeniuzia ametathimishwa kufanya hiyo kazi?

Amesema lengo kubwa la Mamlaka kuwataka watu hawa kuwa na leseni ni kumlinda mtumiaji wa hizo huduma(mlaji).Unapoenda kununua kifaa chako hakikisha umepewa risiti na sasa risiti hiyo imeongezewa kazima iwe na Efd ya TRA, lazima uwe na garantiii kama kunatokea lolote uweza kufidiwa kile kifaa na kupatiwa kingine hiyo ndiyo nia njema ya serikali kuweka huo utaratibu. Alisema

Amesema baadhi ya mafundi wanapotengeneza vifaa vya wateja wao asilimia kubwa wanabadilisha namba tambulishi na kupewa namba ya mtu mwingine ambapo amesema hilo ni tatizo.Kwa usalama wa nchi hili swala la msingi sana najua namba ya simu kitamvulishi ni kitambulisho muhimu kwa watumiaji wa simu hivy kuweni makini, hata vocha mnapozitumia msizitumie hovyo. Alisema
Muwezeshaji wa Warsha hiyo Injinia Jan Kaay (TCRA) akiendekea kutoa elimu kwa washiriki.
Wakwanza kulia ni mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqqaro ndiye akiyefungua warsha hiyo ya siku moja ya watumishi na viongozi mbalimbali wa serikali mkoani Arusha katika ukumbi wa Goldenrose.
Baadhi ya washiriki wa warsha hiyo wakiendelea kufuatilia kwa makini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...