Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola, akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Kamulebya, Kata ya Butimba, Jimbo la Mwibara, Wilayani Bunda Mkoa wa Mara, wakati Mbunge huyo alipofanya ziara katika kijiji hicho kusikiliza kero za wapigakura wake pamoja na kuwahamasisha kuanza maandalizi ya kilimo kwa kuwa msimu wa kilimo umeshafika. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 
Mkazi wa Kijiji cha Kamulebya, Kata ya Butimba, Jimbo la Mwibara, Wilayani Bunda Mkoa wa Mara akimuuliza swali Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola (hayupo pichani), wakati Mbunge huyo alipofanya ziara katika kijiji hicho kusikiliza kero za wapigakura wake pamoja na kuwahamasisha kuanza maandalizi ya kilimo. Lugola aliwapa nafasi wananchi kutoa kero zao ndani ya Jimbo lake. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola (kulia), akimsikiliza Afisa Tarafa ya Kenkombyo, Rebeca Mdodo alipokua anatoa taarifa ya Tarafa yake kwa Waziri Lugola, kabla ya Mbunge huyo hajaanza kuzungumza na wananchi wa Kijiji cha Bulamba, Kata ya Butimba, Jimbo la Mwibara, Wilayani Bunda Mkoa wa Mara. Lugola ameanza ziara jimboni humo leo akisikiliza kero za wapigakura wake pamoja na kuwahamasisha kuanza maandalizi ya kilimo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...