Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.
Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) akiteta jambo na Gavana wa Benki
Kuu ya Tanzania, Prof. Frolens Luoga, nje ya viwanja vya Bunge, Jijini,
Dodoma, baada ya kukutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti,
kujadili Muundo na Maudhui ya Muswada wa Sheria ya Huduma Ndogo za
Fedha ya Mwaka 2018, unaotarajiwa kuwasilishwa Bungeni siku chache
zijazo.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Bajeti, Mhe. David Silinde (Mb), akimwonesha Waziri wa Fedha na
Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), kijitabu cha Sera ya Taifa ya
Huduma Ndogo za Fedha, wakati kamati hiyo ilipokutana na Waziri huyo,
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Adelardus Kilangi (Mb) na Gavana wa
Benki Kuu ya Tanzania Prof. Florens Luoga, kujadili Muundo na Maudhui ya
Muswada wa Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya Mwaka 2018,
utakaowasilishwa kwa hati ya Dharura katika Bunge linaloendelea Jijini
Dodoma
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Bajeti Mhe. Geroge Simbachawene (Mb), akizungmza jambo wakati
kamati yake ilipokutana na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip
Isdor Mpango (Mb), Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Dkt. Adelardus
Kilangi (Mb) na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga, na
wataalamu wa Sera na Uchumi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini
Dodoma, kujadili Muundo na Maudhui ya Muswada wa Sheria ya Huduma Ndogo
za Fedha ya Mwaka 2018.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Bajeti, Mhe. Andrew Chenge (Mb) na Prof. Anna Tibaijuka (Mb)
wakifuatilia kwa makini mjadala wa Muundo na Maudhui ya Muswada wa
Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya Mwaka 2018, unaotarajiwa kuwasilishwa
na Wizara ya Fedha na Mipango, Bungeni, Jijini Dodoma, siku chache
zijazo.
Mjumbe wa Kamati ta Kudumu ya
Bunge ya Bajeti Mhe. Hussen Bashe, akichangia hoja wakati kamati hiyo
ilipokutana na Uongozi wa Wizara ya Fedha na Mipango, na Mwanasheria
Mkuu wa Serikali, kujadili Maudhui ya Muswada wa Sheria ya Huduma Ndogo
ya Fedha ya Mwaka 2018, unaotarajiwa kuwasilishwa Bungeni wakti wa
vikao vya Bunge vinavyoendelea Jijini Dodoma
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia), Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Dkt. Adelardus Kilangi (Mb) (katikati) na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga, wakiandika hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, kuhusu Muswada wa Sheria Ndogo za Fedha unaotarajiwa kuwasilishwa Bungeni Jijini Dodoma, siku chache zijazo.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...