TECNO, miongoni mwa kampuni bora za simu ulimwenguni imezindua rasmi TECNO camon 11 ikiwa ni mwendelezo wa toleo la simu za TECNO camon. Simu za TECNO camon zimekuwa zenye ushawishi mkubwa sana kutokana na uwezo wa kamera na muonekano wake kwa ujumla, na katika uzinduzi huo TECNO ilitoa tamko rasmi kuhusiana na zoezi la ubadilishaji wa simu za camon kwa camon 11 mpya ikiwa imeambatana na ofa ya GB 15 kwa miezi mitatu bure kutoka Vodacom Plc.
Na kama haukua unafahamu TECNO camon 11 ni simu ya kwanza ya TECNO kuwa na teknolojia ya AI kwenye kamera za pande zote mbili zenye kubeba pixel 16 mbele na 13+2 nyuma, na kioo chenye notch. 
Muonekano wa nje wa TECNO camon 11 unaofahamika kama ‘diamond fire design’ unaifanya camon 11 kuwa simu yenye kuvutia zaidi kati ya zote. Na japokuwa ni simu ya kwanza kuzalishwa na kampuni ya TECNO yenye teknolojia mpya katika kioo inayofahamika kama ‘notch’ lakini bado TECNO imehakikisha inaongeza mvuto katika simu hiyo kwa umbo jembamba lenye upana wa nchi 6.2HD+ na uwiano wa 19:9.
Mteja akibadilisha simu ya camon x kwa camon 11 katika duka la TECNO Smart Hub Kariakoo.
Zoezi zima la ubadilishaji wa simu za TECNO camon (camon cx, camon cx air, camon cm, camon x na x pro) linafanyika katika mikoa sita katika maduka ya TECNO yenye promosheni ambayo ni TECNO exclusive Bus Terminal, TECNO Triple B, TECNO Exclusive CCM Babadi Arusha shop, TECNO Exclusive China Plaza Smart Hub, TECNO Exclusive Mlimani City Smart Hub, TECNO Exclusive Samora Smart Hub, TECNO Exclusive Pablo Dodoma, TECNO Exclusive Mbeya Muna Shop, TECNO Exclusive Jambo Mwanza Shop na TECNO Exclusive Tabora Shop.
Ofa hii ya ubadilishaji wa simu za camon kwa camon 11 litakuhitaji kufika kati ya maduka hapo juu ukiwa na simu ya TECNO camon na mshiko kidogo ili uweze kupatiwa camon 11 mpya na ofa ya GB 15 kuanzia sasa hadi tarehe 30 ya mwezi huu wa sikukuu za Christmas.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...