Ni baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na dawa za kulevya kilogramu 3.03

 Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii

MAHAKAMA Kuu Kitengo cha Uhujumu Uchumi jijini Dar  es Salaam, imemuhukumu Mwanamke mmoja  wa Msumbiji Ana Moisie Chissano kifungo cha maisha  baada ya kupatikana na hatia  katika  shtaka  la kukutwa na kilogramu 3.03 za dawa za kulevya aina ya cocaine Hydrochloride.

Mshtakiwa  amefungwa chini  ya kifungu cha sheria cha 15(1)(b) cha sheria namba 5 ya 2015 cha sheria Kuzuia na kusababisha na kupambana na dawa za kulevya.

Hukumu  hiyo imesomwa leo Desemba 12, 2018 na Jaji Lilian  Mashaka baada upande wa mashtaka kuweza kuthibitisha mashtaka hayo pasipo Kuacha shaka baada ya kuridhika na ushahidi  wa mashahidi sita wa  upande wa mashtaka waliofika mahakamani  hapo kutoa ushahidi wao.

Aidha Mahakama  imeamuru dawa hizo za kulevya kuteketezwa kwa utaratibu unaostahili.
 Mshtakiwa Ana Moisie Chissano raia wa Msumbiji  aliyehukumiwa kifungo cha maisha  baada ya kupatikana na hatia  katika  shtaka  la kukutwa na Kg 3.03 za dawa za kulevya aina ya cocaine Hydrochloride.
Pichani kati ni Mshtakiwa  akiwa  katika ukumbi wa wazi wa Mahakama Kuu Kitengo cha mafisadi akisubiri kusomewa hukumu yake

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...