*Yawataka Watanzania wakiwamo wanaCCM kupuuza uzushi, uchonganishi na fitna
*Kamati Kuu kukutana Desemba 17 na 18 Dar, yazungumzia pia ushindi wa kishindo 

Na Said Mwishehe, Globu ya jamii

CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) kimesema kuwa kimefuatilia kwa ukaribu mjadala unaoendelea kwenye mitandao ya kijamii  kuhusu wito ambao umetolewa na Katibu Mkuu wao Dk.Bashiru Ally kwa kada wa Chama hicho Benard Membe kama sehemu ya utaratibu wa kawaida wa Katibu Mkuu kukutana na viongozi na wanachama wa CCM katika kuendelea kuimarisha umoja na mshikamano.

Taarifa ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM Humphrey Polepole ambayo ameitoa leo Desemba 3 mwaka huu wa 2018 amesema kuwa wanatoa rai kwa rai kwa watanzania kuwa wito wa Katibu Mkuu ulikuwa ni wa kawaida wa kiongozi wa CCM kwa mwanachama wa CCM, hivyo uzushi, uchonganishi, fitina na uvumi mwingine wowote unaoendelea hasa katika mitandao ya kijamii na baadhi ya magazeti yenye hila mbaya, wana CCM na Umma wa watanzania wanaombwa 
waupuuze.

"Chama Cha Mapinduzi kinawataka wana CCM na watanzania kwa ujumla kuendelea kuwa na umoja, mshikamano na upendo zaidi katika kipindi hiki ambacho Rais Dk.John Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM anandelea kutuongoza katika mageuzi makubwa ya kiuchumi na ya kimaendeleo kwa watanzania wote,"amesema Polepole kwenye taarifa hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...