NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kinaendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za Pembejeo za kilimo katika maeneo mbali mbali nchini. Hayo ameyasema Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla 'Mabodi katika hafla ya kukabidhi Trekta moja lililonunuliwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Machano Othman Said kwa ajili ya wakulima wa kijiji cha Bumbwisudi kilichopo Wilaya Magharibi "A' Unguja.

Dk.Mabodi ameeleza kuwa hatua hiyo ya kuwapatia Pembejeo za kilimo wakulima zitarahisisha shughuli za kilimo, kwani mazao yatapandwa kwa muda mwafaka na kupatikana mavuno mengi. Kupitia hafla hiyo Dk.Mabodi amewapongeza Mbunge wa Jimbo la Mfenesini Mhe.Mhe.Col.Mstaafu Masoud Khamis pamoja na Mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe. Machano Othman Said kwa utendaji wao mzuri wa kutatua kwa wakati changamoto zinazowakabili wananchi.

Aliwambia Viongozi wa Majimbo mengine kuiga utendaji huo wa viongozi wa Jimbo la Mfenesini kwani wameendelea kutekeleza kwa ufanisi Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020, kwa nia ya kutimiza ahadi walizotoa kwa wapiga kura wao katika Uchaguzi Mkuu uliopita. Aidha aliwataka wananchi wa vijiji mbali mbali vilivyomo katika Jimbo hilo na Majimbo jirani walitumie vizuri Trekta hilo ili lidumu kwa muda mrefu na kulima mashamba mengi ya wakulima.
 BAADHI ya Wana CCM na wananchi waliohudhuria katika hafla ya kukabidhi Trekta moja lililonunuliwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Machano Othman Said kwa ajili ya wakulima wa kijiji cha Bumbwisudi kilichopo Wilaya Magharibi "A' Unguja.
 MBUNGE wa Jimbo la Mfenesini Col.mstaafu Masoud Khamis akizungumza na wana CCM pamoja na wananchi kwa ujumla hafla ya kukabidhi Trekta moja lililonunuliwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Machano Othman Said kwa ajili ya wakulima wa kijiji cha Bumbwisudi kilichopo Wilaya Magharibi "A' Unguja.
 MWAKILISHI wa Jimbo la Mfenesini Mhe.Machano Othman Said akizungumzia maendeleo yaliyopatikana katika Jimbo hilo hafla ya kukabidhi Trekta moja lililonunuliwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Machano Othman Said kwa ajili ya wakulima wa kijiji cha Bumbwisudi kilichopo Wilaya Magharibi "A' Unguja.
 MWENYEKITI wa Mkoa Mjini Magharibi Talib Ali Talib akizungumza katika hafla ya kukabidhi Trekta moja lililonunuliwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Machano Othman Said kwa ajili ya wakulima wa kijiji cha Bumbwisudi kilichopo Wilaya Magharibi "A' Unguja.
NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdulla Juma Mabodi akizungumza na wananchi mbali mbali waliohudhuria katika mkutano hafla ya kukabidhi Trekta moja lililonunuliwa na Mwakilishi wa Jimbo hilo Machano Othman Said kwa ajili ya wakulima wa kijiji cha Bumbwisudi kilichopo Wilaya Magharibi "A' Unguja.
 
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...