NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi, amesema CCM imendelea kusimamia kwa ufanisi sera za maendeleo kwa jamii bila kujali itikadi za kisiasa. Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na Watendaji wa Baraza la Manispaa Mjini, huko Sebleni katika mwendelezo wa ziara yakeb ya kukagua miradi mbali mbali iliyotekelezwa na manispaa chini ya mfumo wa Ugatuzi.

Dk.Mabodi ameeleza kwamba mipango endelevu inayotekezwa na Serikali za mitaa kwa lengo la kuimarisha huduma muhimu za kijamii katika nyanja za afya,elimu,uvuvi,ufugaji,kilimo na ujasiriamali ni kwa ajili ya wananchi wa rika zote bila ya kubaguliwa. Ameeleza kuwa Serikali Kuu imeamua kupeleka madaraka katika Serikali za Mitaa kwa lengo kurahisisha upatikanaji wa huduma bora za kijamii kwa wananchi.

Ameeleza kwamba utekelezaji mzuri wa mipango iliyomo katika ugatuzi ndio litakuwa ni chimbuko la utengenezwaji wa Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2020/2025, iliyokuwa bora na inayoendana mahitaji halisi ya wananchi. Pamoja na hayo amewasihi Watendaji wote waliotolewa Serikali Kuu na kupelekwa Serikali za mitaa kuendelea kuwa wazalendo wenye kujituma kwa moyo mmoja katika kuhudumia jamii.

Kupitia ziara hiyo Naibu Katibu Mkuu huyo, aliitaka Manispaa hiyo kuhakikisha miradi mbali mbali inayotelezwa inakuwa ndio vipaumbele halisi vya wananchi husika katika maeneo yao na inakuwa na viwango vinavyokubalika kisheria.
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi  akielekea  katika ukaguzi wa ujenzi wa jengo la kisasa la machinjio ya kuku katika Soko la Darajani.
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi akipokea maelezo juu ya maendeo yaliyofikiwa katika ujenzi wa jengo la soko la kuku darajani.
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi akikagua shamba la mboga mboga la kikundi cha shehia ya Nyerere iliyopo katika Wadi ya Amani ambao wanajishughulisha na kilimo na wanasaidiwa na Manispaa ya Majini katika kazi zao.
 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi (kushoto) akipokea maelezo kutoka kwa Afisa  Muunguzi  Ashura Amour Mwinyi (kulia)  wa Kituo cha Mamama  Wajawazito na Watoto cha Sebleni akielezea huduma za Afya zinazotolewa bure katika kituo hicho zikiwemo za kipimo cha Ultra Sound.
NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi akipewa maelezo ya mashine maalum ya kusaga taka taka za kutengenezea mbolea ya mimea huko katika kikundi cha ujasiriamali kilichopo Shauri Moyo Zanzibar , katika ziara yake ya kukagua miradi inayotekelezwa na Manispaa ya Mjini chini ya ugatuzi.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...