Na Baba Faisal

MWENAMUZIKI maarufu kwenye muziki wa kizazi kipya ambaye anafanya kazi zake chini ya Lebo ya WCB Rajab Abdul Kahali a.k.a

Harmonize ameamua kuachia wimbo wake mpya wa Paranawe ambao tayari umeanza kuwa gumzo kwenye vituo mbalimbali vya redio pamoja na mitandao ya kijamii.

Unajua kwanini wimbo huo umeanza kuwa gumzo ?Ukweli ni kwamba licha ya wimbo huo kuwa una siku mbili tangu kuachiwa rasmi na msanii huyo umekuwa gumzo kwasababu Harmonize kupitia wimbo huo amethibitisha yeye ni moja kati ya wasanii bora kutokana na aina ya staili yake anayotumia katika kuimba na nyimbo zake.

Kikubwa ambacho kimeongeza ladha ya wimbo wa Paranawe ni pale ambapo ameamua kumshirikisha Rayvany ambaye kwa hakika sauti yake imefanikiwa kupenya kwenye masikio ya mashabiki wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania.Hivyo Harmonize a.k.a Konde Boy ameamua kumpa nafasi Rayvany katika wimbo huo.

Ni jana tu ndio Harmonize ameachia wimbo huo ambao tayari umeshika kasi mtaani.Kama unavyojua tena kwenye bodaboda huko mtaani tayari wameshaweka kwenye flash zao na kilichobaki wanasikiliza mdundo huo wa Paranawe kama sehemu ya kuwa na watu wa kwanza kuusikiliza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...