Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
UTITIRI wa kodi ambazo zinalipwa na wawekezaji nchini bado umeonekana kuwa changamoto kubwa kwao na hivyo kutoa ombi kwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk.John Magufuli kuangalia namna ya kupunguza utitiri huo wa kodi ambao umekuwa mzigo kwao pamoja na wananchi kwa ujumla.
Ombi hilo limetolewa Mjini Dodoma na Mkurugenzi wa Ushirikiano na Uhusiano wa Jamii wa Kampuni ya Cetewico Limited Katrin Boehl baada ya baadhi ya maofisa wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT) pamoja na waandishi wa habari wa habari za fedha na uchumi kufanya ziara ya kutembelea kampuni hiyo kama sehemu ya mafunzo kwa vitendo.Waandishi hao wapo kwenye mafunzo ya kuandika habari za fedha na uchumi yaliyoandaliwa na BoT ikiwa ni muendelezo wa mkakati wa kuwajengea uwezo waandishi wa habari nchini.
"Kwa upande wangu lazima niseme nimeona ushirikiano wa hali ya juu katika Serikali yangu Dodoma kwani nikiwa na tatizo lolote ninakwenda katika ofisi za Serikali yangu ya Dodoma, hivyo imeonesha uthamini wa kiwango kikubwa wa kazi tunazofanya" ameongeza Katrin.
Amesema kampuni yao inapongeza juhudi za Serikali katika ujenzi wa Tanzania ya viwanda nchini ili kufikia uchumi wa kati na wamedhamiria kuunga mkono kwa vitendo kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu lakini changamoto kubwa ambayo wanakabiliana nayo ni uwepo wa kodi nyingi ambazo zinawafanya wanakuwa katika wakati mgumu kutekeleza majukumu yao ya uzalishaji kwai gharama ni kubwa.
UTITIRI wa kodi ambazo zinalipwa na wawekezaji nchini bado umeonekana kuwa changamoto kubwa kwao na hivyo kutoa ombi kwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk.John Magufuli kuangalia namna ya kupunguza utitiri huo wa kodi ambao umekuwa mzigo kwao pamoja na wananchi kwa ujumla.
Ombi hilo limetolewa Mjini Dodoma na Mkurugenzi wa Ushirikiano na Uhusiano wa Jamii wa Kampuni ya Cetewico Limited Katrin Boehl baada ya baadhi ya maofisa wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT) pamoja na waandishi wa habari wa habari za fedha na uchumi kufanya ziara ya kutembelea kampuni hiyo kama sehemu ya mafunzo kwa vitendo.Waandishi hao wapo kwenye mafunzo ya kuandika habari za fedha na uchumi yaliyoandaliwa na BoT ikiwa ni muendelezo wa mkakati wa kuwajengea uwezo waandishi wa habari nchini.
"Kwa upande wangu lazima niseme nimeona ushirikiano wa hali ya juu katika Serikali yangu Dodoma kwani nikiwa na tatizo lolote ninakwenda katika ofisi za Serikali yangu ya Dodoma, hivyo imeonesha uthamini wa kiwango kikubwa wa kazi tunazofanya" ameongeza Katrin.
Amesema kampuni yao inapongeza juhudi za Serikali katika ujenzi wa Tanzania ya viwanda nchini ili kufikia uchumi wa kati na wamedhamiria kuunga mkono kwa vitendo kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu lakini changamoto kubwa ambayo wanakabiliana nayo ni uwepo wa kodi nyingi ambazo zinawafanya wanakuwa katika wakati mgumu kutekeleza majukumu yao ya uzalishaji kwai gharama ni kubwa.
Waandishi
wa habari wakiwa pamoja na maofisa wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT)
wakimsikiliza Mkurugenzi wa Ushirikiano na Uhusiano wa Jamii wa Kampuni
ya Cetewico Limited Katrin Boehl wakati anafafanua namna kampuni yao
inavyotengeneza mvinyo unaotokana na zabibu ya Dodoma.Waandishi na
maofisa hao wametembelea kampuni hiyo kama sehemu ya mafunzo kwa
vitendo.
:Mwenyekiti
wa mafunzo ya waandishi wa habari za uchumi na fedha Nurdin Selemen
(kulia) akijadiliana jambo na Mkurugenzi wa Ushirikiano na Uhusiano wa
Jamii wa Kampuni ya Cetewico Limited Katrin Boehl wakati wa waandishi wa
vyombo mbalimbali walipotembelea kwenye kampuni hiyo.
Mkurugenzi
wa Ushirikiano na Uhusiano wa Jamii wa Kampuni ya Cetewico Limited
Katrin Boehl akiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari za
fedha na uchumi na maofisa wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT) baada ya
kutembelea kampuni yake kuangalia shughuli za uzalishaji.
Meneja
Msaidizi Uchumi na Takwimu wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT) Kanda ya Kati,
Dk. Zegezege Mpemba akizungumza mbele ya Mkurugenzi wa Ushirikiano na
Uhusiano wa Jamii wa Kampuni ya Cetewico Limited Katrin Boehl() baada ya
waandishi wa habari walioko kwenye mafunzo ya habari za fedha na uchumi
kutembelea kampuni hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...