Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo- Mtwara

Serikali imeagiza korosho zote inazonunua kwa wakulima kupitia Bodi ya Nafaka na Mazao mchanganyiko kuanza kubanguliwa nchini.

Agizo hilo la serikali limetolewa na Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) leo tarehe 8 Disemba 2018 wakati akizungumza kwenye Mkutano wa wamiliki wa viwanda vya kubangua korosho kwenye ukumbi wa mikutano kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.

Hasunga alisema kuwa Mkakati wa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Mhe Dkt John Pombe Magufuli ni kuwanufaisha wakulima nchini hivyo maamuzi ya kununua korosho ni sehemu ya maamuzi mema kwa manufaa ya wakulima wote.

Alisema wakati serikali inaendelea kukamilisha uhakiki wa wakulima wa korosho pamoja na kuendelea na malipo ya wakulima mpaka hivi sasa tayari wakulima 77,380 wamekwishalipwa hivyo hakuna korosho itakayoruhusiwa kusafirishwa kwenda nje ya nchi bila utaratibu maalumu badala yake korosho zote zitabanguliwa nchini.
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akizungumza kwenye Mkutano wa wamiliki wa viwanda vya kubangua korosho katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara leo tarehe 8 Disemba 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Kushoto ni Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akijadili jambo na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe Joseph Kakunda (Mb) wakati wa Mkutano wa wamiliki wa viwanda vya kubangua korosho katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara leo tarehe 8 Disemba 2018.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe Joseph Kakunda (Mb) akizungumza kwenye Mkutano wa wamiliki wa viwanda vya kubangua korosho katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara leo tarehe 8 Disemba 2018. 
Kushoto ni Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stella Manyanya (Mb), Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof Joseph Buchweshaija na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe wakifatilia Mkutano wa wamiliki wa viwanda vya kubangua korosho katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara leo tarehe 8 Disemba 2018

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...