WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola ametangaza kufungua miradi mikubwa mitano ya maendeleo jimboni kwake, Wilayani Bunda, Mkoa wa Mara ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa katika mikutano yake kwa wananchi wa jimbo hilo siku za nyuma. Lugola amesema tayari mipango imepangwa katika kufanikiwa miradi hiyo inafunguliwa jimboni humo ikiwa ni hatua ya kuondoa umaskini kwa wananchi na kuliletea mafanikio makubwa jimbo hilo na Wilaya ya Bunda kwa ujumla, 

Akizungumza na Wananchi wa Kata ya Namhula, Wilayani humo, leo, Lugola alisema mradi mkubwa wa Maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kwa ajili ya kumwagilia mazao mbalimbali ikiwemo zao la mpunga katika Bonde la Namhula tayari wataalamu wamefika kulipima bonde hilo pamoja na kuanza mchakati wa mradi huo, pia uwepo wa maji hayo yatasaidia kumwagilia mazao mengine ya nafaka jimboni humo. 

“Mradi mwingine ni wa ufugaji wa kuku wa kienyeji na tuna mashine kubwa za kuangulia vifaranga, maandalizi yapo tayari na eneo la ufugaji huo utakua shule ya Msingi Magunga Kata ya Neluma, pia mradi wa ufugaji wa ng’ombe nyati na ufugaji huo pia utafanyika Sekondari ya Neluma katika Kata hiyo hiyo, na pia tutakuwa na ufugaji wa samaki katika mabonde,” alisema Lugola.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola (kushoto) akizungumza na Wananchi wa Kata ya Namhula, Jimboni humo, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, leo. Lugola alitangaza kufungua miradi mikubwa ya maendeleo jimboni humo hivi karibuni. Kulia ni Mfanyabiashara wa Chakula cha Samaki cha Aluzola, Saimon Katolilo, ambaye aliitwa na Mbunge huyo kutoa elimu kuhusu bidhaa hiyo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola akizungumza na viongozi wa Kata ya Muranda, Jimboni humo, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, leo. Lugola alitangaza kufungua miradi mikubwa ya maendeleo jimboni humo hivi karibuni. Kulia ni Diwani wa Kata hiyo, Jogolo Biswalo, na kushoto ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Muranda, Juma Mapole. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...