Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameitaka Jamii kubadili fikra kwa kuchunguza na kufikiria jinsi ya kutumia vipengele mbalimbali vya lugha ya Kiswahili na Utamaduni wake kama bidhaa ya biashara.

Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la Nne la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama Cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani (CHAUKIDU) na kuratibiwa na Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA). “Sote ni mashahidi wa namna lugha ya Kiswahili imeendelea kukua kwa kasi na kuwa si lugha tena bali ni bidhaa yenye tija katika soko la utandawazi” alisema Makamu wa Rais.

Kaulimbiu ya Kongamano hilo la siku mbili inayosema KISWAHILI CHETU UMOJA WETU KWA MAENDELEO YETU limehudhuriwa na wadau na wataalamu kutoka Mataifa ya Uingereza, Poland, Marekani, Misri, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda, Pakistan Ujerumani na Austria. Makamu wa Rais ameipongeza CHAKIDU kwa kuhakikisha Kiswahili hakimezwi na lugha za kigeni na kukifanya kiendelee kukita mizizi kwa kusambaa maeneo mbalimbali.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Nne la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani (CHAUKIDU) katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) kampasi ya Vuga. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 
 Sehemu ya Wadau na Wataalamu wa Kiswahili waliohudhuria  ufunguzi wa Kongamano la Nne la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani (CHAUKIDU) katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) kampasi ya Vuga. 
Watoto wa Skuli ya Kisiwandui wakipendezesha Kongamano kwa kuimba nyimbo ya Mwanandege wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Nne la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani (CHAUKIDU) katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) kampasi ya Vuga.
 Baadhi ya Vitabu mbalimbali vilivyoonyeshwa leo wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Nne la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani (CHAUKIDU) katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) kampasi ya Vuga.  (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...